Wednesday, April 30, 2014

HII NAYO KALI,JAMAA AMWAGIWA KINYESI NA MTUHUMIWA WAKATI AKITOKA MAHAKAMANI



Mkazi  wa Kata ya Ngara mjini wilaya ya Ngara mkoa wa Kagera, Bw, Philimoni Bunziya akimwelezea mwandishi wa habari hizi jinsi alivyomwagiwa chupa yenye kinyesi na
mtuhumiwa wakati akitoka Mahakamani katika maeneo hayo.

DSC04588

Na Daniel Makaka, Ngara

 MKAZI mmoja wa Kata ya Ngara mjini wilaya ya Ngara mkoa wa Kagera, Bw. Philimoni Bunziya alijikuta akishambuliwa na chupa iliyokuwa na kinyesi karibu na nyumbani kwake alipokuwa akitoka mahakamani.

 Tukio hilo limetokea leo Aprili 28 mwaka huu majira ya saa 4 asubuhi  katika mji wa Ngara ambapo Bwana huyo aliposhambuliwa  kwa kutupiwa chupa ya maji iliyokuwa  imetapakaa kinyesi cha binadamu  kwa kupigwa mgongoni kwake  na mtu aliyemfahamu.

Amesema kuwa baada ya kufanyiwa kitendo hicho alichukua chupa hiyo na kuelekea kituo cha Polisi cha mjini Ngara kwa lengo la kipata msaada zaidi  juu ya swala hilo  na baada ya kufika hapo alitoa maelezo na kupewa RB.NAMBA.NGR/IR/337/2014. Kw ajili ya mtu huyo aweze kukamatwa na kujibu tuhuma zinazomkabili.

 Bw. Bunziya amesema kuwa tangu aliporipoti Polisi hadi sasa mtu huyo aliyemfanyia kitendo hicho ambaye alimtaja kwa jina kuwa ni Bw, Mohamed Khalfani ambaye ana asili ya kiarabu mkazi wa Ngara mjini hajachukuliwa hatua yoyote ya kukamatwa au kuhojiwa juu ya tuhuma hizo na amelitupia lawama Jeshi la Polisi wilaya ya Ngara kwa kushindwa kuchukua hatua.

Alieleza kuwa ameshangazwa na Jeshi la Polisi wilayani humo kushindwa kumkamata bwana huyo huku akiwa anafahamika wazi  kwa kumtaja kuwa yeye ndiye aliyefanya kitendo hicho cha kumtupia chupa hiyo.

Hata hivyo Bw.  Mohamed Khalfani alipoulizwa na waandishi wa habari juu ya tuhuma hizo alikanusha na kusema yeye hajafanya kitendo hicho kwa kuwa hana ugomvi wowote na Bw. Bunziya hivyo anashangazwa na tuhuma hizo nzito.

Naye  Mkuu wa wilaya ya Ngara Bw, Costantini Kanyasu amesema kuwa hana taarifa na tukio hilo na kusema kwa kuwa yeye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ya Ngara hivyo atafuatia na kuhakikisha swala hilo  hilo linapatiwa ufumbuzi.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Bw. George Mayunga amesema hana taarifa juu ya swala hiyo na kusema atalishughulikia ili mtuhumiwa huyo akamatwe ili ajibu tuhuma hizo zinazomkabili.

No comments:

Post a Comment