Friday, March 7, 2014

MAINDA ATESWA NA PETE ALIYOVALISHWA NA MAREHEMU MAX



Stori: Gladness Mallya
STAA  wa filamu  za Kibongo, Ruth Suka ‘Mainda’ amejikuta akikumbuka pete aliyovishwa na aliyekuwa mchumba wake, marehemu Saidi Banda ‘Max’ na kusema ataendelea kumuombea kwani alikuwa ni mwanaume aliyekuwa na malengo makubwa kwake.

Ruth Suka ‘Mainda’.
Mainda alifunguka hayo kupitia mtandao mmoja wa kijamii na kusema kuwa kila akiziona picha za siku alipovishwa pete ya uchumba, anajikuta akitokwa na machozi.
“Miaka inakimbia sana miss u so much...! Kama ndoto vile, siku ile sitaki kuikumbuka ila kwa yote namshukuru Mungu.
“Asante Saidi kwa sababu ulionyesha kuwa una malengo makubwa na mimi mpaka  sasa ningekuwa naitwa Mrs, upendo wako kwangu bado upo sanaa ila hilo ulilolianzisha kwenye kidole changu japo ndoto haikukamilika kupitia wewe litatendeka, asanteni wote mlioshiriki siku ya hili tukio akiwemo Nina na Dotnata,” aliandika  Mainda.

No comments:

Post a Comment