Tuesday, January 14, 2014

HII NDIO STORY KAMILI KUHUSU UJAUZITO WA WEMA NA ALIYEMPA MIMBA HIYO..!!

 

MSANII maarufu wa Bongo Movie, mrembo na mwenye pesa pengine kuwazidi wengi na ambaye hivi karibuni amezua mijadala mikubwa baada ya kurudiana na mpenzi wake wa zamani Diamond, ambaye pia ni maarufu katika muziki wa kizazi kipya nchini na mwenye kuongoza kwa mapato nchini, imegundulika kuwa ana ujauzito wa miezi kadhaa.

Wema ambaye alishindwa kuficha hisia zake na hatimae kuweka kuandika kwenye mtandao wa kijamii wa instagram,” …mmmmmh jamani hichi kitumbo… hakifichiki now…” kuashiria kuwa mabadiliko ya mwili yameshaanza kuonekana (Picha chini inaonesha ujumbe huo kamili).

Mtandao wa huu ulianza kuhisi taarifa hizo na kuamua kuzifuatilia kwa karibu ili kujua nini haswa kinaendelea au ni hisia tu. Ndipo mwandishi alipochukua jukumu la kumtafuta mlimbwende huyo Wema Sepetu na kugonga mwamba.


Hata hivyo jitihada hizo hazikuishia hapo ndipo kilipopatikana chanzo cha karibu na Wema na kudai kuwa “ amekuwa akilalamika mabadiliko hayo na hata kusikika akisema anaihisi ameconsive…” kilisema chanzo hicho bila kutaka kutambulika hadharani.
“Ni kweli itakuwa hivyo na ndio maana Diamond aliamua kumtangaza rasmi siku hile ya chrismas” aliongeza.

Diamond ambaye alimtupilia mbali mpenzi wake Penny na kurudiana na Wema mapenzi yao hayakufichika kwani wakiwa China walipiga picha za mahaba na kuziweka kwenye mitandao ya kijamii na kuzua hisia tofauti.

Hivi karibuni wamekuwa karibu sana kimapenzi na kuamua kuonesha siri zao za ndani bila kuficha, “mwenye macho haambiwi ona… juzi tu wameweka video zao wakiwa kitandani kila mtu ameziona, lakni pia Diamond kumnunulia nyumba baada ya kusikia mkataba wake umeisha na kwamba hautoongezwa, na mambo mengine kibao” kiliongeza chanzo hicho

“lakini tusubiri miezi tisa tu sio mingi na mimba huwahaifichiki bana tutaona

No comments:

Post a Comment