Tuesday, November 12, 2013

REST IN PEACE DR MVUNGI


Sengondo Mvungi 1 
Habari za kusikitisha zilizotufikia jioni hii zinasema kuwa Dk. Sengondo Mvungi amefariki dunia katika Hospitali ya Milpark Afrika Kusini alikokuwa akitibiwa. Dk. Mvungi alipelekwa wiki iliyopita Nov. 7 kwa ajili ya kupewa matibabu zaidi akitokea Hospitali ya Muhimbili kitengo cha Moi ambako muda wote alikuwa hajitambui baada ya kushambuliwa na majambazi na kuumizwa vibaya sehemu ya kichwani akiwa nyumbani kwake Kibamba

Ni jana tu ambapo Waziri wa mambo ya ndani Dr. Emmanuel Nchimbi alitangaza kushikiliwa kwa watu tisa wanaotuhumiwa kuhusika na ujambazi uliofanywa dhidi ya Dr. Sengondo Mvungi aliekua mjumbe wa Tume ya Marekebisho ya Katiba Mpya na kiongozi wa NCCR-Mageuz. 


Inauma sana!!! Taifa letu tuzidi kuliombea sana na tusikate tamaa!!!

MAASINDA INATOA POLE KWA FAMILIA YAKE NA WATANZANIA WOTE KWA UJUMLA

No comments:

Post a Comment