Tukio la mauaji hayo lilitokea saa 6
usiku wa kuamkia juzi baada ya wauaji kuvamia familia hiyo na kisha
kuingia ndani ya chumba alimokuwa amekala kikongwe huyo.
Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha
Kasang'hwa, Maganiko Ndiomali, alisema wauaji walimkata kwa mapanga
kikongwe huyo kichwani,mikono na kwenye matiti.
Alisema pamoja na mayowe yaliyopigwa
na watoto wa marehemu ili kuomba msaada, juhudi za wananchi kuwasaka
wauaji hazikuzaa matunda.
Kuna madai kuwa kikundi
kinachohusishwa na mauaji hayo kimekuwa kikodiwa na baadhi ya watu ili
kulipiza kisasi baada ya kufiwa na ndugu zao wakiamini kwamba wamerogwa.
Kikundi hicho kinadaiwa kuhusika na
mauaji ya kikatili dhidi ya Mondesta Nchambi (53) mkazi wa kitongoji cha
Isabilo wilayani Chato kwa kumchinja mithili ya kuku.
Kamanda wa polisi mkoani Geita,Leonard
Paulo alithibitisha kuwepo kwa matukio hayo lakini alisema hadi sasa
hakuna mtu au watu waliokamatwa wakihusishwa na mauaji hayo.
Chanzo:mwananchi mtandaoni
Tuesday, October 8, 2013
WACHINJAJI WAMCHINJA KIKONGWE KWA MAPANGA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment