
Awali, ilidaiwa Ramadhan alikuwa na tabia ya kuwachukua watoto wadogo wa mtaani hapo na kuondoka nao na kuwarudisha baadaye, kitu kilichowafanya wazazi wa mtoto huyo kutokuwa na wasiwasi.

Mtuhumiwa wa utekaji.
Wakizungumza na mwandishi wetu, wazazi wa mtoto huyo walisema
waliamua kutoa taarifa polisi na kufunguliwa jalada nambari
KJM/RB/8994/13 baada ya kupashwa kuwa mtekaji ambaye alishaacha kazi
yake ya kukaanga chipsi, aliondoka muda mrefu na binti yao na hakukuwa
na dalili za kurejea.Baada ya kuhangaika kwa muda mrefu, wazazi hao pamoja na majirani walifanya uchunguzi wa chinichini na kufanikiwa kupata namba ya simu ya mtekaji huyo, lakini walifanikiwa kubadilishana naye ujumbe mfupi wa simu kwani hakuwa akipokea simu yake ya kiganjani.
Ads not by this site

Ads not by this site

Mtoto Maryment Ibrahim aliyetekwa na Ramadhan.
Wazazi hao walisema kuwa Oktoba 19 mwaka huu mmoja wa majirani
walioguswa na tukio hilo aliyejitambulisha kwa jina la Justin Henry
alijitolea kusafiri mpaka Gairo kumsaka mtoto na mtekaji wake jambo
ambalo lilifanikiwa kwa kumpata mtoto akiwa mzima wa afya japokuwa
mtekaji alishtukia na kukimbia.
No comments:
Post a Comment