By GAMBISHI DWESE
Yawezekana kweli Bwana Domy umekutana nami. Mimi
Ndiyo PAPA-DIMAYO 1: GAMBISHI DWESE,( nabii wa kwanza wa DIMAYO) hata
hivyo pengine umeninukuu kimakosa.Kwanza kabisa Dimayo haiamini katika
uwepo wa mungu muumbaji aliye hai wala aliyekufa anayedaiwa kuhusika na
kila kinachoendelea ulimwenguni.
Na nimeshatoa kitabu kinachoitwa HAKIKA HAKUNA MUNGU MUUMBAJI ALIYE HAI
WALA ALIYEKUFA anayehusika na kila kinachoendelea. kijitabu hiki
kinaeleza kinagaubaga kwanini Dimayo haiamini katika uwepo wa mungu
muuumbaji. nikipata nafasi nitakiingiza kwenye mtandao ili watu wengi
wakisome.
Ni kweli hakuna kitu Dhambi bali kuna makosa. na kosa linaweza kuwa kosa
kulingana na mazingira na wakati katika jamii tofauti. Na ni kweli
kwamba dini yetu ni ya starehe wala si ya mateso, maana tunaamini hakuna
maisha zaidi ya haya tuliyonayo. Dimayo haijampa mtu ruksa ya kuvunja
kanuni halisi asili wala sheria halali ya serikali yake halali na wala
haina upotoshaji hata kidogo.
Kinachoitwa sadaka kwetu huwapa watu wenye matatizo. Ni kweli kuna
michango mingine lakini ni ya hiari na ni kwa ajili ya ushirika. Ni
kweli kwenye JUMADI (jumba la makutano la Dimayo kutakuwa na kaunta ya
vinywaji). unajua kunywa na ulevi ni vitu viwili tofauti; ulevi ni tabia
ya mtu ya kutumia vileo kupindukia, lakini kwetu tunasema kunywa
uwezavyo ilimradi huumii wala kuumiza vyote kisaikolojia na kimwili, kwa
mantiki hiyo ulevi kwetu noma ila unywaji ni safi.
Uchawi ni sayansi, ila utumike kwa faida siyo kwa kuleta madhara.
kuwaambia watu eti acheni ngono eti mungu hapendi wataacha?. wambie
wafanyeje ngono kulingana na wakati na mazingira. Dimayo inamfundisha
mtu kutenda inavyofaa yanayofaa kutendwa kwa kufuata kha na kahaka.
Anyway nashukuru kwa kuianzisha mada hii, nafikiri nitachukua nafasi
kuielezea zaidi kila inavyowezekana. Nina uhakika kwa mtu yeyote mwenye
uwezo mkubwa wa kutumia akili zake hawezi kupingana hata kidogo na
DIMAYO.
Source: JF
No comments:
Post a Comment