Thursday, October 31, 2013

BABA KANUMBA AMPIGA MARUFUKU MAMA KANUMBA KULITAJA JINA LA KANUMBA

Katika hali ya kushangaza, baba wa aliyekuwa msanii maarufu wa filamu Bongo, marehemu Steven Kanumba, Charles Kanumba amempiga marufuku mama mzazi wa msanii huyo, Flora Mtegoa kutumia jina la Kanumba kwa namna yoyote.

Mzee Charles Kanumba.

Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni baba Kanumba alisema mama Kanumba hana mamlaka ya kulitumia jina la Kanumba kwani hana uhusiano nalo.
“Mimi ndiye mwenye mamlaka na jina la Kanumba kwa sababu ni la kwangu lakini namshangaa mama Kanumba kuendelea kulitumia jina hilo hata kwa watoto wasionihusu kama mtoto wa mwanaye aliyezaliwa hivi karibuni na kuitwa Kanumba Junior.
“Anahusiana nini na hilo jina wakati huyo siyo damu yangu, yeye ana baba yake kwa nini asitumie jina lake, sitaki kabisa atumie jina langu mwanangu ameshafariki na mimi ndiye mwenye mamlaka ya kutumia hilo jina,” alisema mzee huyo.
Akilizungumzia suala hiyo, mama Kanumba alisema: Sitaki kumsikia kabisa,kama vipi aende mahakamani.”

No comments:

Post a Comment