Thursday, May 30, 2013

GSK YAZINDUA KAMPENI YA KUHAKIKI DAWA KWA KUTUMIA SIMU

Naibu Waziri akizungumza machache Kabla ya Kuzindua Kampeni ya Kuhakiki dawa kwa njia  ya kutuma ujumbe Mfupi wa Simu kampeni iliyopo katika Kampuni ya Kusambaza dawa ya  Glaxo Smith  Kline (GSK) iliyofanyika leo katika Hoteli ya Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.


Kampuni Maarufu Nchini na Duniani ya Kusambaza Dawa leo imezindua  kampeni mpya ya Kusambaza Dawa zake ambapo itamuwezesha Mteja au Mgonjwa kupata Uhakika wa Dawa Hizo.
Akizungumza katika Uzinduzi huo Mkurugenzi wa Mradi DK William Mwatu amesema kuwa, Kampeni hiyo itamuwezesha Mteja kuhakiki dawa kwa kusoma  namba maalum iliyopo katika Dawa zake na kutuma katika namba maalumu kwa kutumia simu yake ya Mkononi  ili waweze kuletewa ujumbe wa Uthibitisho kuwa Dawa hiyo ni halalai.
Dk Mwatu amesema kuwa  katika Uchunguzi wao walioufanya kwa baadhi ya Watanzania na wagonjwa mbalimbali wamebaini kuwa  Watanzania wengi hawana uhakika na Madawa wanayoyatumia kwa kuhofia kuwa madawa hayo sio halali.
Kwa upande wake Naibu waziri wa Afya Dk Seif s Rashid  amesema kuwa , kutokana na  Kampeni hiyo wanaamini kuwa uingizwaji haramu wa Madawa Feki utapungua kama si kwisha kabisa na wagonjwa watafaidi Mfumo huo Mpya wa kuhakiki Madawa.
Dk Seif ameitaka GSK kuwa na Ukaribu zaidi na Mamlaka ya Chakula na Dawa ili waweze kushirikiana  kwa ufasaha  na kuboresha Afya za Watanzania.
Dk Mwatu amesema kuwa,  Mteja atakapo nunua dawa,  anatakiwa kuifungua kwanza kasha kusoma Namba maalum iliyopo katika Dawa hiyo baada ya kungwangua Mithili ya Vocha  na Kuituma namba hiyo katika Namba  15629 ambapo Mitandao inayotumika ni Voda, Tigo, Zantel na Airtel.

Hii ndiyo Nembo ya Kampeni iliyozinduliwa leo na Naibu waziri wa Afya

Naibu waziri wa  Afya  Dk Seif Rashid akifungua dawa inayosambazwa na Kampuni ya GSK  ili kutuma ujumbe Mfupi wa Kupata uhakika wa Dawa kabla ya Kutumia amabapo baadaye alitumiwa Ujumbe Mfupi wa kuwa Dawa hiyo ni  Halali nani Mali ya GSK. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mradi Dk William Mwatu.

No comments:

Post a Comment