Monday, March 4, 2013

WAZIRI KIGODA AZINDUA BODI MPYA YA TBS, AIPA MIEZI SITA KULETA MABADILIKO

Waziri Kigoda (kushoto) akijadiliana jambo na Prf Mhilu

Waziri wa viwanda na biashara Dr Abdala Kigoda amezindua bodi mpya ya shirika la viwango Tanzania (TBS)ambapo ameipa bodi hiyo miezi sita kupitia mwenyekiti wake Prof.Cuthbert Mhilu kuhakikisha kuwa tbs inarudi katika hali yake ya ubora kama zamani.
Akizungumza katika uznduzi wa bodi hiyo uliofanyika katika ukumbi wa tbs hivi leo,Waziri Kigoda alisema kua karibu asilimia 90 ya bidhaa zinazoingizwa nchini hazina ubora na kua walaji wanatumia bidhaa chache zenye ubora hivyo amewataka wajumbe wa bodi hiyo kuhakikisha kuwa wanapambana na tatizo hilo kwa haraka.
“Natoa miezi sita kwako mwenyekiti wa bodi hii hakikisha kua tbs inatoa ubora unaokubalika na kurudi katika hali yake  ya zamani”,amesema  Kigoda.
Aidha waziri amezungumzia suala la uajiri wa wafanyakazi tbs na kusema kuwa tbs ina wafanyakazi wachache kulingana na nchi nyingine kama Kenya ambapo wanawafanyakazi wa tbs  zaidi ya elfu moja wakati Tanzania ina wafanyakazi kati ya mia nne na mia tano tu jambo ambalo linachangia kuzorota kwa shirika hilo.
 
Kwa upande wake mwenyekiti wa bodi hiyo Prof.Cuthbert  Mhilu amempongeza waziri kwa kuvunja bodi iliotangulia kutokana na kutoridhishwa na ufanisi  pamoja na utendaji  mbovu katika shirika hilo na kuahidi kua katika menejimenti yake atahakikisha kua kutakuwepo na mabadiliko katika shirika hilo na kuwa watazingatia nia ya wizara katika kuzindoa bodi mpya ndani ya kipindi hicho cha miezi sita.

No comments:

Post a Comment