Tuesday, March 5, 2013

UCHAGUZI MKUU NCHINI KENYA MATOKEO YA AWALI YANAONYESHA KUWA UHURU KENYATTA ANAONGOZA


Kura zikihesabiwa
Baada ya siku ndefu ya watu kupiga kura nchini Kenya, wengi wana hamu kujua rasmi mshindi wa uchaguzi wa urais. Hata hivyo matokeo ya mwanzo yameanza kutolewa na tume ya uchaguzi na mipaka Kenya, IEBC.
Matokeo hadi kufikia saa kumi na mbili jioni yalikuwa yanaonyesha Uhuru Kenyattaakiongoza dhidi ya mpinzani wake Raila Odinga. Matokeo kutoka sehemu mbali mbali yalichelewa hasa kwa sababu ya hitilafu za kimitambo.
Na hivi ndivyo mambo yalivyokuwa. Endelea kutoa maoni yako kwenye ukurasa wetu wa 
Bofya Bofya
17:31Ng'endo Angela aliye katika eneo bunge la Othaya anasema kuwa Mary Wambui amemrithi rais mstaafu Mwai Kibaki kama mbunge wa eneo bunge la Othaya baada ya miaka 39 ya Kibaki kuwa mbunge wa eneo hilo. Kibaki alikuwa amempendeka Mugambi Manyara kuwa mrithi wake, lakini ameshikilia nafasi ya tatu
17:29 Matokeo ya mwanzo mwanzo ya kura za urais yaliyotolewa sasa hivi kutoka kwa tume ya uchaguzi yanaonyesha kuwa Raila Odinga ana kura 2,133,202 wakati Uhuru Kenyatta ana kura 2, 718,021
17:05 Kwa sasa Raila Odinga ana kura 2, 107, 670 wakati Uhuru Kenyatta akiwa na kura 2,697,056
17:02 Vigogo wa Muungano wa CORD wake Raila Odinga wamesema kuwa licha ya matokeo kuonyesha bado wako nyuma, wafuasi wao wasiwe na wasiwasi kwani kura nyingi zingali kuhesabiwa. Mgombea mwenza wake Kalonzo Musyoka amewaambia wapiga kura kupitia televisheni kuwa wawe watulivu wasubiri matokeo kutoka kwa tume ya uchaguzi
15:00 Matokeo kufikia sasa ni kwamba Uhuru Kenyatta amepata kura2,606,617 wakati Raila odinga ana kura 2,011,869
14:31 Hadi kufikia sasa kulingana na matokeo yanayotolewa na Tume huru ya uchaguzi Kenya ni kuwa Uhuru Kenyatta amepata kura 2,534 019wakati Raila Odinga akiwa na kura 1,939,549. Haya ni matokeo ya mapema tu
13:05 Abdulkarim Taraja akiwa Mt Elgon, anasema kwenye 
Bofya
facebookkuwa anafurahi ambavyo wanaoshindwa wanakubali matokeo ya kura katika eneo hilo

12:59 Blessed Kuriah anasema kwenye ukurasa wa 
Bofya Bofya
bbcswahili, kuwa hali ni tulivu katika eneo bunge la Gatundu Mkoa wa Kati

12:57 Uhuru Kenyatta 2,484,760 Raila Odinga 1,884,152
12:46 Mwandishi wetu Jamuhuri Mwavyombo akiwa mjini Mombasa anasema mji umetulia, maduka mengi yangali yamefungwa watu wakiwa na wasiwasi kuangalia hali itakavyokuwa
12:37 Uhuru Kenyatta 2,459,133 Raila Odinga 1,851, 671
12:24 Idadi ya kura kwa wagombea wakuu wa urais Uhuru Kenyatta 2,429,895 Raila Odinga 1,823,384
12:21 Mwandishi wa BBC Ng'endo Angela ambaye yuko katike eneo bunge la Othaya, Mkoa wa kati, shughuli ya kuhesabu kura inarejelewa upya, baada ya mmoja wa wagombea kutaka hilo lifanyike kufuatia madai ya wizi wa kura. Eneo hilo lina ushindani mkubwa ikizingatiwa lilikuwa eneo bunge la Rais anayestaafu Mwai Kibaki na alikuwa amependekeza mmoja wa wagombea kupigiwa kura na watu wa eneo hilo. CHANZO BBC

No comments:

Post a Comment