Katika Kuhakikisha kuwa Unyanyanyasaji kwa walemavu wa Ngozi
unakoma kabisa Ncxhini, Shirika la Under
the same Sun UTSS limezindua
Mradi wa Radio katika kanda ya ziwa ambapo Imani za Kishirikina dhidi ya
Walemavu wa Ngozi (Albinisim) umeshamiri.
Akizungumza Mbele ya Waandishi wa habari, Meneja wa Mradi huo Bi, Rachel Moyo, amesema
kuwa, Mradi huo utakuwa katika Redio
zilizopo Kanda ya Ziwa na Redio hizo zitakuwa na Vipindi vya kuelimisha jamii
vitakavyojulikana kwa jina la Tambua albinisim, na vitarushwa kwa Mtindo wa
Makala mchanganyiko, Majadiliano ya Moja kwa Moja ikiwa ni pamoja na Mchango wa
simu kutoka kwa Wasikilizaji pamoja na Mchezo wa Kuigiza.
Bi, Rachel amesema kuwa Mradi huo umedhamini wa na kwa ushirikiano wa Serikali ya Canada kupitia
Ubalozi wa Canada ambapo walichangia
kiasi cha Dola 20,000 za kimarekani sawa na milioni 30 za Kitanzania.
No comments:
Post a Comment