Saturday, March 9, 2013

ODINGA ASEMA HAYATAMBUI MATOKEO YA URAIS KENYA


Aliyekuwa Mgombea Urais nchini Kenya kwa tiketi ya ODM, Raila Odinga na Waziri Mkuu wa Zamani wa Serikali ya Mwai Kibaki amesema hayatambui matokeo na Ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta.



Odinga amesema hayo wakati akizungumza na wanahabari na halaiki na kushusha lawama zake kwa tume Huru ya uchaguzi ya IEBC kuwa imerudia madudu ya mwaka 2007 ambayo yaliingiza nchi katika vurugu kubwa.



“Kamwe hatuwezi kuyatambua matokeo hayo yaliyotangazwa hivi punde, hivyo tumeamua kwenda Mahakamani kudai haki ya wakenya Walio wengi kisheria”.

No comments:

Post a Comment