Friday, March 15, 2013

CHELSEA YAIBANJUA STEAUA BUCHAREST NA KUTINGA ROBO FAINALI EUROPA LEAGUE

 Ugomvi dimbani: Mshambuliaji Fernando Torres wa Chelsea, akilalamikia mbele ya mwamuzi baada ya kuchanika na kuanza kutokwa na damu kutokana na kupigwa na mchezaji wa Steaua Bucharest. Chelsea ilishinda mechi hiyo ya marudiano kwa mabao 3-1 na kufuzu robo fainali kwa jumla ya mabao 3-2.

 Chukua hiyooo; Mshambuliaji Juan Mata wa Chelsea. Juu; akipiga shuti kufunga bao la kwanza la timu yake. Chini; akishangilia bao hilo.
 Hatari hapa, namna gani huyu; Raul Rasescu wa Bucharest (kulia), akiruka juu kujaribu kuwania mpira na David Luiz wa Chelsea.
 Raha ya mechi bao; Wachezaji wa Chelsea wakishangilia bao.
 Aaahhhh wapi!!!!! Mlinda mlango wa Chelsea, Petr Cech akishindwa kuzuia shambulizi lililozaa bao pekee la Bucharest katika mechi hiyo.
 Tunampenda/tunamuhitaji; Mashabiki wa The Blues wakimpigia chapuo la mkataba mpya wa usajili kiungo-mchezeshaji wa timu yao, Frank Lampard.

 Bao la ugenini; Wachezaji wa Bucharest wakishangilia bao ambalo liliwapa matumaini ya kusonga mbele.
 Kisicho riziki, hakiliki; Furaha yao haikudunmu sanam, kwani bao la Torres likatosha kuisukuma timu yao nje ya michuano, huku Chelsea ikifuzu robo fainali Ulaya.
 Nafunga kama hivi; Nahodha wa Chelsea, John Terry, akiruka juu kupiga kichwa kilichoipa timu yake bao la pili.
  Chezea JT Wewee!!! Hapa Terry akishangilia bao lake.
 Elininhooooooooo!!! Juu; Torres akipiga shuti kufunga bao la tatu la Chelsea. Katikati; akishangilia bao hilo kwa kunyoosha mikono juu. Chini akipongezwa na beki Ashley Cole.

No comments:

Post a Comment