Wednesday, March 6, 2013

AFISA WA POLISI AJERUHIWA KWA BOMU HUKO KENYA

Watu ambao  hawajafahamika waliwarushia bomu maofisa usalama waliokuwa wanailinda lango la kuingilia kwenye kituo cha kuhesabia kura katika mji wa Wajir Jumanne usiku (tarehe 5 Machi), na kumjeruhi polisi mmoja anayefanya kazi katika idara ya ukaguzi wa ndani.

Washambuliaji hao walilenga bwalo la halmashauri ya wilaya ya Wajir muda kama wa saa 2:00 usiku, Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Wajir James Mutungi aliiambia Sabahi. Alisema ofisa aliyejeruhiwa alikuwa miongoni mwa maofisa waliosambaza katika eneo hilo kuimarisha usalama katika bwalo hilo, ambapo kura za jimbo la Wajiri Mashariki zinahesabiwa hapo.

Alisema Bomu hilo lilirushwa muda mfupi baada ya Mbunge wa Wajiri Mashariki kutangazwa kuwa mshindi.

"Polisi wanachunguza shambulio hilo lakini hakuna aliyekamatwa," Mutungi alisema.

Mratibu wa Tume ya Uchaguzi na Mipaka kwa jimbo la Wajir Mashariki Andrew Njoroge alisema alikuwa akijitayarisha kutangaza matokeo ya nafasi za urais, magavana, useneta na wawakilishi wa wanawake wakati mlipuko huo ulipotokea.

"Ni kutosikia vizuri na sitaeleza mahali halisi ilikotokea hadi maofisa usalama waifanye hapo kuwe salama," alisema Mratibu huyo,  akiongeza kwamba tukio hilo halikuzuia tangazo hilo.

Chanzo Mitandao

No comments:

Post a Comment