Saturday, January 5, 2013

MEYA AWASHAURI WANANCHI KULIPA KODI

Meya wa Manispaa ya Kinondoni Bw, Yusuph Mwenda (aliyenyoosha mkono) akiongozana na Maofisa wengine Kutoka Manispaa ya Kinondoni leo kwenye Ziara yake ya Kutembelea Ujenzi wa Barabara Mya ya kutokea Ubungo kwenda Makoka jijini Dar es Salaam.
 
Wananchi wa Manispaa ya Kinondoni wametakiwa kulipa Kodi kwa Uaminifu kwani pesa hizo zinatumika katika kazi mbalimbali katika jamii ya Manispaa ya kinondoni.



Hayo yamesemwa leo na Meya wa Manispaa ya Kinondoni Bw, Yusuph Mwenda, wakati alipo fanya Ziara ya Kutembelea Bara bara Mpya Inayojengwa ya Kwenda Ubungo Makoka Jijini Dar es Salaam ambapo katika Maradi huo Nyumba Tisa Zimebomolewa ili kupisha Ujenzi wa Barabara hiyo na Nyumba hiyo Zimelipiwa Fidia ya Shilingi Milioni 187.

Mwenda amesema kuwa, Pesa hizo kiasi cha Shilingi 187 Milioni zimetokana na Wananchi wa waaminifu wanaolipa Kodi na hivyo amewataka Wananchi waendelee kulipa Kodi.

“Naomba wananchi wa Kinondoni waelewe kabisa namna kodi zao zinavyotumika, Fidia hizi zimetokana na Wananchi kulipa kodi hivyo nawataka wananchi wote walipe kodi ili Ziweze kuwasaidia wenyewe”, amesema Mwenda.

Hii ndiyo Barabara Mpya ya Ubungo Makoka aliyoitembelea Meya leo, katika Barabara hii tayari zimebomolewa nyumba Tisa zilizokuwa maeneo haya na kulipiwa Fidia

Engineer wa Manispaa ya Kinondoni akifafanua jambo juu ya namna Mradi utakapo kwenda Mbele ya Mstahiki Meya
Tupo Ziarani japo kuna Matope

No comments:

Post a Comment