Mahakama
ya Wilaya ya Mwanakwerekwe mjini Zanzibar leo imepunguza masharti ya
dhamana kwa Viongozi saba wa Jumuiya mbili za Kiislamu Zanzibar,
wanaokabiliwa na mashtaka ya kusababisha vurugu na kupelekea uharibifu
wa miundombinu ya barabara mjini Zanzibar, leo tena wameshindwa kupata
dhamana.
Afisa Habari Mkuu wa Jeshi la Polisi Zanzibar Inspekta
Mohammed Mhina, amesema kuwa uamuzi huo umetolewa na Hakimu wa
Mahakama hiyo Mh. Ame Pinja, baada ya kukubali maombi ya Mawakili wa
Watuhumiwa waliomba kupunguzwa kwa masharti hayo kwa wateja wao.
Watuhumiwa hao ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maimam ZanzibarSheike Farid
Hadi Ahamed na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Uamsho Sheikh Mselem Ali
Mselemu na wenzao watano.
Inspekta Mhina amesema kuwa kutokana
na uamuzi huo, kila mshitakiwa sasa atatakiwa kuwa na wadhamini
wawili ambao ni watumishi wa Serikali na kwa kila mmoja awe na kiasi cha
shilingi 500,000 tofauti na mashrti ya awali ya wadhamini watatu na kwa
kila mmoja kwa kiasi cha shilingi milioni moja kwa kila mmoja.
Hata hivyo pamoja na kupunguzwa kwa masharti hayo, hakuna hata
mshitakiwa mmoja aliyedhaminiwa kutokana na kukosekana kwa wadhamini
ambao ni watumishi wa serikali.
Inspekta Mhina amesema kuwa
Watuhumiwa hao ambao wanakabiliwa na kesi tatu tofauti za kuzusha ghasia
na kupelekea vurugu katika maeneo mbalimbali ya mji wa Zanzibar,
wamerudishwa rumande hadi desemba 4, mwaka huu kesi yao itakapotajwa
tena.
Amesema wakati wote kesi hiyo ikiendelea, hali ya
ulinzi nje na ndani ya Mahamakama uliimarishwa vya kutosha ambapo
Makachero wa Jeshi la Polisi pamoja na Askari wa Kikosi cha Kutuliza
Ghasia na wale wa vikosi vya Ulinzi vya Zanzibar walikuwepo kuhakikisha kuwa ulinzi unaimarika.
Watuhumiwa hao ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maimam ZanzibarSheike Farid Hadi Ahamed na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Uamsho Sheikh Mselem Ali Mselemu na wenzao watano.
Inspekta Mhina amesema kuwa kutokana na uamuzi huo, kila mshitakiwa sasa atatakiwa kuwa na wadhamini wawili ambao ni watumishi wa Serikali na kwa kila mmoja awe na kiasi cha shilingi 500,000 tofauti na mashrti ya awali ya wadhamini watatu na kwa kila mmoja kwa kiasi cha shilingi milioni moja kwa kila mmoja.
Hata hivyo pamoja na kupunguzwa kwa masharti hayo, hakuna hata mshitakiwa mmoja aliyedhaminiwa kutokana na kukosekana kwa wadhamini ambao ni watumishi wa serikali.
Inspekta Mhina amesema kuwa Watuhumiwa hao ambao wanakabiliwa na kesi tatu tofauti za kuzusha ghasia na kupelekea vurugu katika maeneo mbalimbali ya mji wa Zanzibar, wamerudishwa rumande hadi desemba 4, mwaka huu kesi yao itakapotajwa tena.
Amesema wakati wote kesi hiyo ikiendelea, hali ya ulinzi nje na ndani ya Mahamakama uliimarishwa vya kutosha ambapo Makachero wa Jeshi la Polisi pamoja na Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia na wale wa vikosi vya Ulinzi vya Zanzibar walikuwepo kuhakikisha kuwa ulinzi unaimarika.
No comments:
Post a Comment