Tuesday, November 27, 2012

MAADHIMISHO YA SIKU YA ZIWA VICTORIA YAFANYIKA JIJINI MWANZA

Pichani chini ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Eng.Christopher Sayi (aliyesimama)
akifungua Warsha maalum ya Viongozi kuhusu hifadhi ya Mazingira ya

Bonde la Ziwa Victoria katika Hotel ya Golden Crest Mwanza. Warsha hii

inawajumuisha Viongozi mbalimbali toka Wilaya na Mikoa inayozunguka

Bonde la Ziwa Victoria wakiwemo Waheshimiwa Wabunge,Wakuu wa Wilaya

pamoja na Wataalamu wa Maji,Mazingira na Kilimo. Kulia kwake ni BI

Mwamvua Jilumbe Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu..Wa kwanza kulia ni

Mkuu wa Wilaya ya Kwimba ambaye alimuakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza

Mhe. Eng.Evarist Ndikilio
Baadhi ya  Wajumbe waliohudhuria Semina hiyo.Kushoto  ni Mbunge
wa Bariadi Mashariki Mhe John Cheyo na wa kwa kwanza kushoto walioketi

ni Mkuu wa Wilaya  Meatu Jaquiline Liana
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Eng.Christopher Sayi akisikiliza kwa
makini mada kuhusu utunzaji wa Mazingira katika Semina ya Viongozi

kuhusu hifadhi ya Mazingira ya Bonde la Ziwa Victoria iliyofanyika

katika Hoteli Golden Crest Jijini Mwanza. Kulia kwake ni Mhe. Dr

Kamani Mbunge wa Busega na wa kwanza kulia ni Bi Mwamvua Jilunde

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu. Warsha hii ni sehemu ya Maadhimisho

ya Siku ya Ziwa Victoria itakafikia kilele chake tarehe 29 Novemba

mjini Bariadi.

                       Picha zote Nurdin Ndimbe (Wizara ya Maji)
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Eng.Christopher Sayi akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa mkutano huo mara  baada ya kuufumgua rasmi.

No comments:

Post a Comment