Noti mpya amabazo inatumika hivi sasa nchini Tanzania |
Wananchi hao pia wanachomoa ufito huo na kuchanganya na sigara au tumbaku ambapo hudai hulewa haraka.
Hali hiyo ambayo imeambatana na uadimikaji wa noti hizo, imeshika kasi eneo la Kijiji cha Maleza, Kata ya Kipeta,Wilaya ya Sumbawanga Vijijini, vile vile kwenye vijiji vya Kilangawana na Kamsamba.
Wananchi kadhaa ambao hawakupenda majina yao kutajwa, wamethibitisha kutokea kwa matukio hayo na kuitaka Serikali na Benki Kuu kuchukua hatua za haraka ili kukomesha vitendo hivyo.
Katika hali ya kuhalalisha noti hizo zilizoharibiwa wahalifu hao hutumia gundi kwa kutumia uzi wa mifuko ya mbolea ili ziendelee kutumika.