Sunday, July 22, 2012

WACHAKACHUZI WA KAZI ZA WASANII WAZIDI KUKAMATWA DAR..

Kampuni  ya Msama Promotions, imekamata watu watatu wanaotuhumiwa kuuza kazi za wasanii kinyume na taratibu.
Akizungumza na Dira ya Mtanzania, Mkurugenzi wa Msama Promotions,  Alex  Msama (pichani),  alisema kuwa vijana hao walikamatwa katika eneo la Ubungo jijini Dar es Salaam.
WAlitaja majina ya ya waliokamatwa katika tuklio hilo kuwa  ni Malik Sultan, Ally Msangi, Edward Michael na  Sijali Andrew ambao walikuwa na CD feki 322 za wanamuziki mbalimbali na wasanii wengine.  
Msama alisema zoezi la kukamata wezi wa kazi za wasanii linaendelea kwa kufanya uchunguzi katika maeneo sugu ambako hatua inayofuata ni kwa wale wanauza kazi hizo mikononi.
Aidha Msama analishukuru  Jeshi la Polisi kwa ushirikiano wanaoendelea kuutoa kwa timu ya vijana wake wanaosaka wezi wa kazi za wasanii.