Saturday, July 28, 2012

BADO WATANZANIA WA NYAKASANGWE WANAISHI KWA MATESO

Katibu mwenezi wa CCM, Tawi la Nyakasangwe Bw, Benjamin Steven akisistiza jambo wakati alipokuwa akiongea naWaandishi wa habari juu ya unyanyasaji wao dhidi ya Polisi.

Mjumbe wa Kijiji cha Nyakasangwe, Jastin Frank, akisisitiza jambo kuwa hawawezi kukubali kunyanyaswa na polisi wanaotokea kuwanyanyasa hapo kijijini kwao wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Wanakijiji  wa   Nyakasangwe Kata ya  Wazo wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam  wanaiomba serikali iwaangalie na kuwasaidia kuondokana na unyanyasaji  wanaoupata Dhidi ya Polisi wa kupigwa pamoja kufukuzwa katika maeneo yao  huku wakiwaambia kuwa wao ni wavamizi katika maeneo hayo.
Wakizungumza na waandishi wa habari  kijijini hapo wanakijiji hao walisema kuwa wamechoka kuishi kwa kunyanyaswa na polisi bila ya makosa yoyote kwani wanaishi kama digidigi (pasipo kulala) na Kisingizio cha wao kunyanyaswa ni kwamba  hawatakiwi kuishi kwenye maeneo hayo kwakuwa wao si wamiliki halali.
Majengo Majengo ni Mwenyekiti wa kijiji hicho ambapo alisema kuwa Polisi wanakuja kila kukicha kutaka kuwakamata kwa kisingizio kwamba wanakijiji wote wanaoishi maeneo yale ni wavamizi.
Hata hivyo Majengo alisema kuwa, Kesi yao ipo mahakamani na inasubiriwa kutolewa hukumu lakini wanashangaa bado wanakamatwa ovyo na kubambikiwa kesi.
“Kesi yetu hii ipo mahakamani lakini tunashangaa tunazidi kuwindwa na watu wachache, wakishirikiana na Polisi”,alisema Majengo.

Alisema kuwa, Askari hao wanapokwenda kuwakamata, wanatembea  na watu watatu wanaodai kuwa msitu wa  kijiji hicho ni maeneo yao.
Aliwataja watu hao kuwa ni,Datsan Okololo, Omary Ponchi pamoja aliefahamika kwa jina moja tu la  Mwamasika ambao alidai kuwa ndio wanaoshirikiana na askari wa jeshi la polisi kuwakamata watu kwa madai ya kuwa wao ndio wamiliki halali wa msitu huo wa kijiji hicho.
Naye Katibu Mwenezi  wa CCM  Tawi Nyakasangwe Benjamin Steven, alisema kuwa  viongozi wenzake wote wamekamatwa na polisi na Mpaka sasa Mwenyekiti wake hajulikani alipo baada ya kukimbia askari walipotaka kumkamata.
Akielezea kukamatwa huko kwa viongozi wenzake alisema kuwa,  baada ya uchaguzi uliofanyika  tarehe tano mwezi huu yalikuja magari mawili ya polisi(Defender) zilizofunikwa  na vitambaa vyeusi kwenye ubao wa namba na kuwakamata viongozi wao kwa makosa ya Uvamizi.
“Mimi nashangaa Maswala ya Uvamizi yanaingiliana vipi na Chama, naomba jeshi la Polisi lisichanganye mambo, kwa mambo ya Uvamizi yanamuhusu mwenyekiti wa kijiji na serikali yake na hayawezi kuhusiana na Chama hata siku moja”, alisema Benjamin Steven.
Hata hivyo Mkuu wa wilaya ya Kinondoni  Jordan Rugimana alipoulizwa kuhusiana na sakata hili alisema kuwa kuhusiana na wannchi hao kunynyaswa na kubomolewa nyumba zao kwa kosa la uvamizi ni swala la Mahakama  ndiyo itakayotoa majibu kama wanakijiji hao wanauhalali wa kuishi maeneo hayo au la.
Aidha, kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Kinondoni Charles Kenyela alipoulizwa kuhusiana na swala hilo alisema kuwa, huo ni mkakati wa jeshi la polisi kuendelea kuwakamata wavamizi wa maeneo ya watu.Hizi ndizo namba zao 0714356974,0714573564