Friday, June 8, 2012

NABAKI AFRICA LTD YAMWAGA MIL 15 KW MSHINDI WA DROO YA SHINDA PAA NA NABAKI AFRICAGAWA

 Mkurugenzi mkuu wa Nabaki Africa  Ltd Bw, Hamish Hamilton akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kukabidhi hundi ya kiasi cha shilingi 15,000,000, kwa mshindi wa droo iliyochzeshwa na kampuni hiyo may 31 mwaka huu. Nabaki Africa ilikabidhi hundi hiyo kwa Bw, Kalembo Bisaya ambaye ndiye mshindi wa Droo hiyo ambapo kila mmoja wa wateja walioshiriki shindano hilo alinunua  aidha vifaa vya mfumo wa kuvuna maji ya mvua  vijulikanavyo kama Marley Gutters au mfumo wa kuzuia joto katika paa pamoja na  vigae vya kuezekea aina ya DECRA. Washiriki katika shindano hilo walikuwa jumla ya washiriki 101 ambapo amesema wateja wote ambao wamenunua vigae vya DECRA wataweza kuangalia juu ya mapaa yao na kuona tofauti nzuri ambayo ni DECRA halali tu ndiyo inatoa. Makabidhiano hayo ya hundi yalifanyika katika makao makuu ya Nabaki Africa leo Jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi  mkuu msaidizi wa Nabaki Africa  Ltd Bi Tamia Hamilton akifafnua juu ya utoaji wa zawadi hizo kwa wale wateja waliofanikiwa kushinda katika Droo hiyo.
.
 Mkurugenzi  mkuu msaidizi wa Nabaki Afrika  Ltd Bi Tamia Hamilton (kulia) akimkabidhi mfano wa hundi wa kiasi cha Tsh,  15,000,000/= Bw, Kilembo Bisaya  baada ya kushinda katika droo iliyochezeshwa na kampuni ya Nabaki Afrika LTD .
 Mshindi wa Droo hiyo Bw, Kalembo Bisaya akizungumza na waandishi wa habari juu ya furaha yake baada ya kukabidhiwa hundi hiyo.
Bwana Alison Malopa akifafanua namna ya utoaji wa zawadi baada ya kuelezewa na wakurugenzi kwa lugha ya kingereza.
Mshindi wa droo Bw, Kilembo Bisaya akiwa kwenye picha  ya pamoja na mkewe baada ya kupewa hundi yake.