Friday, May 24, 2013

TBS YAWAPA ONYO WAKANDARASI,, PIA VIWANDA VYA MABATI VIJIHADHARI

Eng Stephen Minja ambaye ni Afisa  Mhakiki kutoka TBS akizungumza na waandishi wa habari wakati wa Maonyesho ya Bodi ya Wakandarasi Tanzania.


Shirika la Viwango Tanzania TBS limewataka Wakandarasi wote Tanzania, kuwa na uhakika na Vifaa vya Ujenzi wanavyovitumia ili kuepusha Athari inayoweza kujitokeza baada ya Kazi yao.

Akizungumza katika Maonyesho ya Bodi ya Wakandarasi Afisa Mhakiki Viwango kutoka TBS Eng Stephen Minja amesema kuwa, ni vyema Wakandarasi wakakagua vifaa vyao kabla ya kuvitumia ili kuhakiki Ubora wa vifaa hivyo na kama vipo katika viwango sahihi.

Eng Minja amesema kuwa, kama Mkandarasi atakuwa na wasiwasi na vifaa vyake ni vyema akawasiliana na tbs ili wakakague wenyewe kupitia wataalamu wake.

Ameendelea kusema kuwa, Shirika la Viwango litahakikisha kuwa  vifaa  vya ujenzi vinavyotumika katika Ujenzi vinakuwa katika kiwango Stahili ambapo Endapo TBS itabaini kuwa kuna Kiwanda kinachozalisha Vifaa ambavyo havipo katika viwango Basi hawatasita Kukifungia Kiwanda hicho.

Ameongeza kuwa tayari Mpaka sasa wameshazifutia leseni Viwanda sita ambavyo vilikuwa vinazalisha Bidhaa ambazo sio stahili, na ametaja Viwanda hivyo kuwa ni Viwanda vitano vya Nondo vilivyokuwa vinafanya Shughuli zake Jijini Dar es Salaam, pamoja na Kiwanda kimoja cha Maji kilichopo Mkoani Tanga.

Aidha Eng, Minja amesema kuwa wanampango wa kufanya Msako wa kushutukiza katika viwanda vinavyozalisha Mabati ili kuchunguza kuwa ni viwanda gani ambavyo havizalishi Mabati yaliyopo katika Kiwango, na endapo watabaini basi watakifungia kiwanda Husika.

Hapa akijibu swali kutoka kwa Waandishi wa habari

No comments:

Post a Comment