Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Kyando Mchechu (kushoto) na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Zebadiah Moshi wakisaini hati za makubaliano. |
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Zebadiah Moshi (kulia), akitoa hutuba fupi kwenye hafla hiyo. |
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Kyando Mchechu (kushoto), akihutubia kwenye hafla hiyo. |
Viongozi mbalimbali wa meza kuu wakiwa kwenye hafla hiyo. |
Vijana watakaopata mafunzo hayo wakiwa katika
picha ya pamoja na watendaji wakuu wa NHC na VETA.
picha ya pamoja na watendaji wakuu wa NHC na VETA.
Vijana watakaopata mafunzo hayo wakiwa katika
picha ya pamoja na watendaji wakuu wa NHC na VETA.
picha ya pamoja na watendaji wakuu wa NHC na VETA.
Mkufunzi wa matumizi wa mashine za Hydraform
kutoka Afrika Kusini, Henry Cockcroft (kushoto),
akielekeza jinsi mashine hiyo inavyofanyakazi.
Mkufunzi wa matumizi wa mashine za Hydraform
kutoka Afrika Kusini, Henry Cockcroft (kushoto),
akimbidhi kitabu chenye matumizi ya mashine hiyo
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa
(NHC), Nehemia Kyando Mchechu.
kutoka Afrika Kusini, Henry Cockcroft (kushoto),
akimbidhi kitabu chenye matumizi ya mashine hiyo
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa
(NHC), Nehemia Kyando Mchechu.
Mkufunzi wa matumizi wa mashine za Hydraform
kutoka Afrika Kusini, Henry Cockcroft (kushoto),
akimbidhi kitabu hicho Mkurugenzi wa Mamlaka ya
Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Zebadiah Moshi.
kutoka Afrika Kusini, Henry Cockcroft (kushoto),
akimbidhi kitabu hicho Mkurugenzi wa Mamlaka ya
Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Zebadiah Moshi.
Vijana watakaopata mafunzo hayo wakipiga makofi
kufurahia mpango huo.
kufurahia mpango huo.
Na Dotto Mwaibale
SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC), limeingia mkataba na Chuo cha Ufundi Stadi (Veta), wa mafunzo maalumu kwa wanafunzi wa chuo hicho ambao watashiriki katika ujenzi wa nyumba za bei nafuu zinazojengwa na shirika hilo maeneo mbalimbali kwa kutumia matofali ya kisasa.
Mkataba huo umefanyika Dar es Salaam leo ukishirikisha viongozi wa NHC na wakufunzi wa Veta kwa niaba ya wanafunzi hao.
Kwa mujibu wa mkataba huo, wanafunzi 35 wamechaguliwa kushiriki mafunzo hayo kwa vitendo, ambapo watashiriki kufyatua matofali kwa kutumia mashine maalumu za umeme na ujenzi wa nyumba hizo utafanyika katika mikoa 14 nchini.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Kyando Mchechu, alisema lengo la kuandaa programu hiyo ni kuhakikisha shirika linanufaisha vijana wanaohitimu mafunzo ya ujenzi na kuingia katika soko la ajira.
Alisema katika mafunzo hayo vijana watajifunza namna bora ya ujenzi kwa kutumia matofali imara yaliyotengenezwa kwa mashine za kisasa za umeme, na kwamba itaboresha elimu yao.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Veta, Zebadia Moshi, alisema chuo kimefurahishwa na hatua hiyo itawezesha vijana hao kuongeza ujuzi zaidi na kupanua soko la ajira.
Moshi alisema kumekuwa na tatizo la ajira kwa vijana wanaomaliza chuo hicho kwani asilimia 66 ndiyo hupata ajira, lakini kuanzishwa kwa programu hiyo kutasaidia kusukuma soko la ajira kwa vijana wengi zaidi wanaohitimu mafunzo chuoni hapo
SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC), limeingia mkataba na Chuo cha Ufundi Stadi (Veta), wa mafunzo maalumu kwa wanafunzi wa chuo hicho ambao watashiriki katika ujenzi wa nyumba za bei nafuu zinazojengwa na shirika hilo maeneo mbalimbali kwa kutumia matofali ya kisasa.
Mkataba huo umefanyika Dar es Salaam leo ukishirikisha viongozi wa NHC na wakufunzi wa Veta kwa niaba ya wanafunzi hao.
Kwa mujibu wa mkataba huo, wanafunzi 35 wamechaguliwa kushiriki mafunzo hayo kwa vitendo, ambapo watashiriki kufyatua matofali kwa kutumia mashine maalumu za umeme na ujenzi wa nyumba hizo utafanyika katika mikoa 14 nchini.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Kyando Mchechu, alisema lengo la kuandaa programu hiyo ni kuhakikisha shirika linanufaisha vijana wanaohitimu mafunzo ya ujenzi na kuingia katika soko la ajira.
Alisema katika mafunzo hayo vijana watajifunza namna bora ya ujenzi kwa kutumia matofali imara yaliyotengenezwa kwa mashine za kisasa za umeme, na kwamba itaboresha elimu yao.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Veta, Zebadia Moshi, alisema chuo kimefurahishwa na hatua hiyo itawezesha vijana hao kuongeza ujuzi zaidi na kupanua soko la ajira.
Moshi alisema kumekuwa na tatizo la ajira kwa vijana wanaomaliza chuo hicho kwani asilimia 66 ndiyo hupata ajira, lakini kuanzishwa kwa programu hiyo kutasaidia kusukuma soko la ajira kwa vijana wengi zaidi wanaohitimu mafunzo chuoni hapo
No comments:
Post a Comment