Fox News wameripoti na kuzianika picha za Washukiwa wa ulipuaji wa mabomu mawili kwenye mbio za Marathon mjini Boston Marekani ambapo watu watatu walifariki na wengine zaidi ya 170 kujeruhiwa.
Hizi hapa chini ni picha pamoja na video zikionyesha washukiwa wawili wanaume ambao FBI inaamini ndio wamehusika na kutega mabomu hayo mawili kwenye sehemu ambayo watu wengi walikuwepo kushuhudia mbio hizo za riadha.
Pamoja na kwamba FBI wamewatambua washukiwa hawa wawili, bado hawajafanikiwa kuwakamata ndio maana wameomba msaada wa Wananchi kutoa taarifa watakapowaona.
No comments:
Post a Comment