Ili kuondoa malalamiko yanayotupwa Serikalini kutokana na vitendo vya
baadhi ya watumishi wasio waaminifu, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya
Dawa (MSD), Cosmas Mwaifwani amesema Serikali sasa imeamua kuweka alama
maalumu katika dawa ambazo watakuwa wakizisambaza kwenye zahanati, vituo
vya afya na hospitali zote nchini kuepusha ubadhirifu ambao hufanywa na
watumishi wasio waaminifu wa Idara ya Afya.
Alama hiyo itakuwepo pia kwenye vidonge na itasaidia kuondoa ubadhirifu huo na vituo vya afya kuwepo na dawa wakati wote.
“Uamuzi
huo umefikiwa baada ya kuwepo kwa malalamiko mengi kutoka kwa wananchi
ya kukosa dawa kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitalini baada ya
kutibiwa na kuambiwa wakanunue katika maduka ya dawa,” alisema.
Alisema
tofauti na kulinda dawa hizo pia alama hizo zitawarahisishia kazi
wakaguzi kwa kugundua uhalifu huo pindi dawa hizo zitakapokutwa katika
maduka ya watu binafsi ya kuuzia dawa.
“Tofauti
na hayo pia alama hizo zitasaidia kutokuingia kwa dawa dhaifu sokoni
ambazo zinadhoofisha afya ya mlaji kwa kuyatia magonjwa usugu,”alisema
Mwaifwani.
Alisema ni jukumu la wananchi kuwa wazalendo na nchi yao kwa kuhakikisha dawa zinazosambazwa na MSD zinatumika kwa walengwa.
Mwaifwani
aliyasema hayo wakati wa semina ya siku moja ya kuhamasisha watendaji
wa sekta ya afya juu ya mpango mpya wa usambazaji wa dawa iliyofanyika
mwishoni mwa wiki.
via HabariLeo
No comments:
Post a Comment