Rais Barack Obama akila kiapo cha kuiongoza nchi ya Marekani muhula wa pili mbele ya familia yake.
Makamu wa rais wa Marekani Joe Biden naye akifanya vivyo hivyo.
Rais
Barack Obama wa Marekani ameapishwa kwa ajili ya muhula wake wa pili
katika hafla iliyohudhuriwa na wanafamilia na waandishi wa habari pekee.
Rais
Obama anaanza muhula wa pili akikabiliwa na matatizo kadhaa nyumbani na
nje, yakiwemo mgawanyiko mkubwa mjini Washington kuhusu masuala
mbalimbali, mpango wa Iran wa nyuklia na wapiganaji wa Kiislamu katika
kanda ya Afrika ya kaskazini.
Sherehe
kubwa inatarajiwa kufanyika leo katika jengo la Capitol mjini
Washington, ambapo hotuba ya Obama inatarajiwa kujikita katika haja ya
kufanya tahfif za kisiasa na warepublican pale inapowezekana.
No comments:
Post a Comment