Monday, January 14, 2013

JESHI LA POLISI MKOA WA KINONDONI LINAWASHIKILIA WATU SABA KWA TUHUMA ZA UHAMIAJI HARAMU NA USAFIRISHAJI WA BINADAMU

Kamanda wa mkoa wa kipolisi wa Kinondoni Charles Kenyela akizungumza na waandishi wa habari leo katika makao makuu ya jeshi la polisi Mkoa wa Kinondoni
 Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni linawashikilia watu 7 kwa tuhuma za kuingia nchini isivyo halali kuwapokea na kuwahifadhi rtaia wa Kigeni isivyo halali.

Akiszungumza na waandishi wa Habari kamanda Kenyela amesema kuwa  tukio hilo limetokea tarehe 09/01/2013 maeneo ya Kimara Bonyokwa kwenye nyumba ya Mtu aliyefahamika kwa Jina la Issa Omary mwenye umri wa miaka 39.
Kamanda Kenyela amesema kuwa wamewakuta watuhumiwa hao wakiwa wamefungiwa kwenye Chumba kimoja  ndani ya nyumba ya Omary na walibaini kuwa watuhumiwa hao wametokea Nchini Ethiopia na wengine wametoka Burundi ambapo wangesafirishwa kwenda Afrika ya Kusini kupitia Mpaka wa Mtwara.

Ameendelea kusema kuwa, wahamihaji hao hawana  hawakuwa na hati ya kusafiria isipokuwa huvushwa mpaka hadi Mpaka na watu maalum walioandaliwa na wasafirishaji(Traffickers)

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Ndayeshimeye Abdulkabir (30) Mrundi mkazi wa Msava Kayanzi ambaye ni Mfanya Bihashara pamoja na Nduwayezi Blaise (24) Mrundi mkazi wa Bujumbura mwanafunzi wa Chuo cha Bridge College ambao hao ndio wahusika wakuu wa Usafirishaji wa wahamiaji haramu wanaotokea Ethiopia.
Hawa ndio wafanya Bihashara wakuu wa kusafirisha Binadamu Ndayeshimye pamoja na Mwenzie Nduwayezi  wakiwa chini ya ulinzi

Watuhumiwa  7 wakiwa chini ya Ulinzi


Huyu ndiye Omary, Mtanzania aliyewahifadhi wahamiaji Haramu

 
Kamanda Kenyela akisema Machache na Wafanya Bihashara ya Usafirishaji Binadamu





No comments:

Post a Comment