![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjJCYEXRCm1LMTHWLl7U4D8nxL6dYcDmtSozD3t4W-HtX8WMdb5T8rA_vLO4hLV09lR0OHUsIzsXAxofhTTm1-Gwb3gBwis3sLRu3FycymeFipsxyJBmcP-76zaGaaCsJ4RqJbmCTC9Pl5E/s640/IMG_1038.JPG) |
Katibu mwenezi na Mahusiano ya Umma wa NCCR-MAGEUZI Mh, Moses Machali (kulia) akimsomea Bw, Edo Makata kadi ya NCCR kabla ya kumkabidhi ili ajiunge rasmi katika chama hicho baada ya kutoka CHADEMA. |
Hatimaye yule kijana ambaye alidaiwa kutimuliwa Chadema
pamoja na kunyan’ganywa Madaraka Bw, Edo R Makata aliyekuwa Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Mbeya ameungana
na chama cha Nccr-MAGEUZI leo katika
makao makuu ya Chama hicho yaliyopo jijini Dar es Salaam.
Katika Mazungumzo yake na waandishi wa habari Bw, Makata ameyataja
machafu mengi anayodai yamemfanya akihame CHADEMA na kuhamia NCCR na kukanusha kutimuliwa
kwake na badala yake alidai amejiuzulu
mwenyewe kutokana na Machafu hayo.
Makete ameyataja baadhi ya
machafu yaliyopo katika chama hicho cha CHADEMA kuwa ni, Ufisadi, Ukabila pamoja na Ubabe wa Mwenyekiti wa Chama hicho
Mh, Freeman Mbowe na kuongeza kuwa Dk Slaa anatumia Fedha nyingi kufanya Ziara
kwa gharama ya CHADEMA pasipo Baraka za vikao halali vya Chama.
MAASINDA ilimuuliza Bw, Makata, kuwa ni kwanini hakuwahi
kuzungumzia Machafu hayo wakati akiwa ndani ya chama na badala yake amesubiri
aondoke ndipo akaamua kuyasema?
Jibu: Siku zote hata katika mahusiano ya Mapenzi mkiwa ndani
ya mapenzi mtavumiliana mabaya yote lakini Mkiachana ndio mtaanza kuyasema yale mabaya pamoja na
siri zote zilizokuwa zinafanyika ndani, hivyo basi mimi nilikuwa navumilia tu
lakini sasa kwasababu nimeondoka ndio maana nimeamua kuyatapika yote.
Bw, Makate alikabidhiwa kadi ya NCCR MAGEUZI rasmi leo na
katibu Mwenezi wa Chama hicho Mh, Moses Machali naye Edo akaikabidhi kadi ya
CHADEMA kwa Mh, Moses Machali .
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiEV_pPp6yfe-FQ9Md_owKJwepsKcm91DJ1K8UipgMjiN4-B8bgWQ3_YMLI8eiKwClm6G6yI8NRg3F7MHYolvTyMiO8joJFF-LGJP690mQ-0-2-rhDIWIrFuEp_KWysSX5GiFP9BdUtqAij/s640/IMG_1037.JPG) |
Baada ya kukabidhiwa kadi ya NCCR Bw, Edo aliamua kuitoa ya Chadema na kumkabidhi Mh, Moses Machali |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgNrwesDp0Xlmz7Q_SfNsctN1AlFf2m5XyG6nHBo2Q0bURxBCEMgNzdz1P-_B877EAaaFig5RnA3KY526zetiZgmLeUaBU3yKetYe4lRyB_U-4Z1KGtg3QvQrbQys9TGzexIB3ybpJn6a2E/s640/IMG_1040.JPG) |
Hapa Bw, Edo akifurahia Kadi yake mpya ya NCCR |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhwmvvfQh3UQAVhLQjREjybuI1ovtd5DAYt1XzVkOOaPWZh8sHbcZypYGZW7BF5Ri0jFJZa9ScFzxOSTP5VdIHKytjG33Ir-MrhawrlHRQtL2B49cs9nYvRIpfarTrdAC-QYuPwAQRmAnHY/s640/IMG_1041.JPG) |
Baadhi ya waandishi wa habari waliokuwemo kwenye mkutano huo wakiwa makini kusikiliza |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiMNFvc-K_IFryyv99YDQRFqxa7slsRCt_WnWdzX9ip07sQYf1e6DpA6JX50_LhwLdr5Ty-LMzsHgRcsIeT3PLoDe342MvsmaNsYgMglZe5i3p7HuMBPcetNfdwm0eyoVJ7tIH2gUhWkoFC/s640/IMG_1048.JPG) |
Hii ndiyo kadi ya NCCR |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgcMlmE6yOKT0w2Nimk6EtbaHZeQOjkTggl8rMez8s2rHoOi5oSTocZumznzoCgAi07iyj7wPCgd1YcrO6x6DhlVtoYWH-bitucalKSwB5-BerHeJlLMuSzXZGzO1spvu8iwsF8uKWNCUDw/s640/IMG_1054.JPG) |
Makata mwenyewe ndani ya kadi ya NCCR |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEguZcmNkvqofJcJaK3GDHHFLNOQlzoYcRhEnxxiaaTzAXUeW7w5NFQrJg1064Ct7R4R7Ma-iY5JWrpt2MdB2gej2jVrwvzuxab-rBohv8N436ECTngc86P4Yk_JIbJkUPSag_YXeUy2xf8-/s640/IMG_1056.JPG) |
Kadi ya CHADEMA aliyoirudisha Bw, Makata |
No comments:
Post a Comment