Thursday, November 15, 2012

DIARY YA LADY JAYDEE KUANZA JUMAPILI

Msanii Mkongwe na anaye endelea Kutamba katika Game hii ya Muziki Mwanadada Judith Wambura maarufu kama Lady JD akizungumza na waandishi wa habari leo katika Hoteli ya Nyumbani Lounch juu ya Kuanzisha Kipindi chake katika Televisheni ya EATV kitakachoitwa Diary ya Lady Jaydee.
 
Kama msanii, Lady Jaydee amefanikiwa na kutambulika katika kiwanda cha muziki ndani na nje ya nchi, huku akitunukiwa Tunzo nyingi zaidi akiwa na albamu zake tano. Pamoja na kuwa anaendelea na fani yake ya muziki, Lady Jaydee ameamua kuwafikia na kuwaburudisha wapenzi wa kazi zake kwa njia nyingine.
Lady Jaydee sasa anaanza sura mpya ya burudani kwa kuleta kipindi cha TV kiitwacho DIARY YA LADY JAYDEE, ambacho kutaonekana katika kituo cha TV cha EATV

Jaydee amesema kuwa kipindi hicho kitakuwa kinaelezea maisha yake halisi kuanzia alipotokea mpaka alipo sasa ambapo amesema kuwa kipindi hicho kitaanza kurushwa Jumapili saa tatu usiku na itakuwa ni kila jumapili muda kama huo huo.

Amewataka Watanzania kufwatilia kipindi hicho ili waone Mafanikio yake na wao waweze kuiga na kufwata Ndoto zao.
Judith Wambura akifafanua Jambo mbele ya waandishi wa habari(hawapo pichani) na anayeonekana kushoto kwake ni Mkuu wa Vipindi vya Kwenye Televisheni EATV Bi, Lyidia Igarabuza

Hapa wakisikiliza maswali kutoka kwa waandishi wa habari

No comments:

Post a Comment