Habari kwa mujibu wa blogu ya Lukwangule --
M AHAKAMA ya Hakimu Mkazi wilaya ya Korogwe jana ilimkataa Mwanasheria
Mkuu wa Serikali kumwakilisha Mkuu wa wilaya ya Korogwe, Mrisho Gambo
katika kesi ya madai ya Shilingi Milioni 96 dhidi yake.
Katika
kesi hiyo Na. 7/ 2012 mlalamikaji ni Mwanasheria wa Halmashauri ya Mji
Korogwe, Najum Tekka anayedai kukashifiwa na Gambo wakati wa kikao cha
Kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya kwamba stashahada ya Sheria aliyopata mtumishi huyo ni ya chupi.
Awali
ilidaiwa kwamba mkuu huyo alimwalika mlalamikaji kutoa ushauri wa
kisheria kuhusu namna ya kumaliza mgogoro baina ya halmashauri ya mji na
wafanyabiashara na kwamba baada ya kufanya hivyo mlalamikiwa alipinga
ushauri uliotolewa na kisha kutoa kauli hiyo kwamba shahada yake ni ya chupi.
Mbele
ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo Hamis Salum, mlalamikaji huyo aliiomba
mahakama imwondoe Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye aliwakilishwa
Mahakamani hapo na Wakili wa Serikali, Rebecca Msalangi kwa kuwa hana
mamlaka katika madai hayo na kamwe Ofisi yake haikuwahi kupeleka ombi
maalum la kutaka kumwakilisha Gambo kwenye shauri hilo.
Kwa
upande wake, Hakimu Mkazi akisoma uamuzi mdogo wa Mahakama kuhusiana na
mabishano hayo alikiri kwamba utaratibu haukufuatwa na kamwe hapakuwa na
ombi la Mwanasheria Mkuu wa Serikali kutaka kumwakilisha Gambo kwenye
madai hayo.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Novemba 14 mwaka huu.