Saturday, October 6, 2012

MWANAFUNZI AKUTWA AMEKUFA CHUMBANI KWAKE

MWANAFUNZI aliyemaliza kidato cha sita katika shule ya sekondari Saronge, iliyoko mkoani Kigoma na kuchaguliwa kwenda chuo kikuu cha UDSM kwa ajili ya kuanza masomo ya mwaka wa kwanza katika kipindi cha mwaka 2012/2013, amekufa akidaiwa kujinyonga wilayani Bunda mkoani Mara.

Tukio hilo lilitokea juzi katika kitongoji cha Kimanitwentemi, kilichoko katika kijiji cha Kabasa wilayani hapa na Mwenyekiti wa kitongoji hicho Donard Kalemela, alisema mwanafunzi huyo anatambuliwa kwa jina la Majinge Mafuru, mkazi wa kijiji hicho.

Baba wa mwanafunzi huyo, Samson Musimu, alisema mwili wa mwanafunzi huyo uligunduliwa na mdogo wake baada ya kutoka shuleni na kuingia ndani ya nyumba hiyo.

Alisema mfukoni mwake walikuta ujumbe wa maandishi ukisomeka, “Naomba mniandalie mahali pa kulala, nimeamua mwenyewe, baada ya kuwa nimeghafirika, msimshuku mtu yeyote, ni maamuzi yangu mwenyewe, ahsante.”


Source: wavuti.com