Monday, October 1, 2012

MANISPAA YA ILALA YAKUSANYA 17.1 BILIONI ZA MAPATO YAKE KWA MWAKA 2011/2012

Meya wa Manispaa ya Ilala Bw, Jerry Slaa akizungumza na wadau mbalimbali pamoja na walipa Kodi  katika kikao kilichofanyika leo Ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Katika kikao hicho meya  aliufahamishaUmma kuwa Manispaa yake imefanikiwa kukusanya kiasi cha 99% cha mapato yake.
Meya amesema kuwa kwa ujumla ukusanyaji wa mapato katika mwaka huu imepanda  kutoka  88% kwa mwaka 2010/2011 mpaka shilingi 17.1 bilioni zilizokusanywa kwa mwaka huu  kiasi ambacho ni sawa ya 99% ya mafanikio ya Malengo.
“Ongezeko hili limetokana na vyanzo vingi vya mapato kwa 102% ambayo ni shilingi 2.25 bilioni kutoka katika mabango ya Matangazo yaliyopo Barabarani” amesema.
Ametaja Kitengo kingine kilichochangia kuongeza mapato kuwa ni Utoaji wa Leseni za Ujenzi kilichochangia Milioni 307 pamoja na  Makusanyo ya Mapato kutoka kwenye kodi yaliyochangia shilingi 2.14 bilioni .

Jerry Slaa akiwa kwenye picha ya Pamoja na wadau mbalimbali waliokuwemo katika mkutano huo

Wadau wakijadiliana jambo