Saturday, October 20, 2012

KAMATI YA OLYMPIKI YATANGAZA UCHAGUZI MKUU WA VIONGOZI WA TOC


Kamati ya Olympiki Tanzania inatarajia kuwa na  Uchaguzi Mkuu wa Viongozi wake wa Ngazi za juu na chini kuanzia Tarehe 8/12/2012 mkoani Dodoma.

Akizungumza na waandishi wa Habari leo jijini Dae es Salaam katika Ofisi za Kamati hiyo, Rais wa TOC Bw, Rashid Gulam amesema kuwa  Uchaguzi huu unaofanyika kwa kipindi hiki ni Muendelezo wa  Uchaguzi kwani Uchaguzi mkuu hufanyika kila Baada ya  Olympiki inapomalizika ina maana kubwa kuwa viongozi wapya watakaochaguliwa wawe na muda muhafaka wa (miaka 4 ) katika maandalizi na timu zetu kwa ushirikiano na Serikali.

Amesema kuwa Mgombea atakayegombea nafasi yoyote anatakiwa awe na sifa zilizopo katika katiba ya TOC ikiwemo Awe mtanzania halisi na anaweza kuongea Kingereza na Kiswahili sawa sawa.

Amewataka wagombea  wenye sifa kwenda kuchukua Fomu katika Ofisi za TOC Tanzania Bara na Zanzibar tarehe 25/10 na kurejeshwa tarehe 15/11 mwaka 2012.

Ameongeza kuwa Fomu zitauzwa  kwa shilingi 200,000(Rais, Makamu wa Rais, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu, Mhazini pamoja na Mhazini Mkuu msaidizi) na shilingi 150,000 kwa wale watakaogombea nafasi za Wajumbe ambapo Fomu zote zitauzwa katika Ofisi za  TOC.