Tetesi zinaeleza kwamba, tukio la kuuawa kwa Kamanda huyo huenda
limesababishwa na uhasama na watu mbali mbali katika maeneo ya kazi
alikowahi kufanyia, na kwamba hilo ni tukio linalotia shaka iwapo kama
imetokea kwa bahati mbaya.
Baadhi ya
watu wanalihusisha tukio hilo na mahusiano ya kimapenzi, misimamo yake
mikali ya kupambana na majambazi, ambapo alikuwa akitoa onyo kwa
majambazi kutoingia katika eneo lake la kazi.
Kwa
upande wao, watoto wa Doroth Moses walisema kwamba siku ya tukio mama
yao aliwaaga jioni kuwa anakwenda katika kikao cha harusi cha rafiki
yake, na wakati anarudi nyumbani majira ya saa 4 usiku aliwapigia simu
ili wamfungulie geti, na kwamba wakati mtoto mmoja Keny Rogers (17),
akienda kumfungulia geti aliona kundi la watu kama watano wakiwa
wamezunguka gari.
“Yule mwanaume (RPC), aliyekuwa amemleta mama (Doroth), sisi hapa hatumjui na hata hatujawai kumuoana.
Lakini mama alitupigia simu akisema tumfungulie geti..
“Wakati
mimi nimeenda kufungulia geti, niliona kundi la watu watano lakini mimi
hawakunioana. Wakati naendelea kuwacheki (kuwaangalia), kama nawafahamu
ama lah, ghafla nikasikia mlio wa bunduki kisha wale watu wakakimbia.
Nikaanza kuona damu nyingi zinamwagika chini”, alisema mtoto Keny.
Awali iliripotiwa kwamba Doroth alikua ni dada wa marehemu Barlow.
Hili
ni miongoni mwa matukio makubwa ambayo yameripotiwa kutokea jijini
Mwanza, ambapo hivi karibuni iliarifiwa kwamba, Ofisa mmoja wa Uhamiaji
Mkoani Mwanza, Albert Buchafwe alinisurika kuuawa kwa risasi na mtu
anayedaiwa kuwa ni Mkuu wa Kituo Kidogo cha Polisi cha Nyakato Mwatex
(OCS), Abubakar Zebo baada ya kushukiwa kuwa ni jambazi.
Ilidaiwa
kwamba, Ofisa huyo wa Uhamiaji alifyatuliwa risasi tano wakati
akijaribu kukimbia, na kwamba gari lake liliumizwa vibaya na risasi
zilizokuwa zikifyatuliwa na OCS Abubakar, na kwamba tukio hilo
lilithibitishwa na Ofisa huyo wa Uhamiaji pamoja na marehemu RPC Barlow.
Tukio jingine lilitokea miezi
michache iliyopita, ni lile la mwanasiasa maarufu jijini hapa, Seni
Manumbu aliyeuawa kwa kupigwa risasi za moto na watu wasiojulikana,
wakati alipokuwa akifunguliwa geti ili aingie nyumbani kwake.
---
Sehemu hii ya taarifa imenukuliwa kutoka kwenye habari ilivyoandikwa na Sitta Tumma kwenye FikraPevu – Mwanza.
-------------- xxxxx----------------
Mwandishi
alifika eneo la tukio na kuzungumza na mtoto wa kaka wa Mwalimu Moses
anayeitwa Kennyrogers Edwin aliyedai kuwa muda mfupi kabla ya tukio,
mwalimu huyo aliwapigia simu akiwataka wamfungulie.
Alipofungua
lango, aliona gari limepaki na watu wawili wakiwa upande wa abiria na
wengine kwa dereva na alisikia mlio wa risasi na kushuhudia watu hao
wakikimbia baada ya kuona pikipiki inakuja nyuma yao.
Mmoja
wa wakazi wa Kitangiri, Edward Jackson ambaye ni mwanafunzi wa kidato
cha tatu sekondari ya Kitangiri alisema akiwa mezani anajisomea usiku
alisikia mlio wa risasi na alipotaka kutoka nje mama yake alimzuia ili
asije akadhurika.
Akizungumzia tukio hilo, Mkuu wa
Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema, licha ya kushitushwa na kuhuzunishwa
na tukio hilo, alitaka wananchi kutoa ushirikiano ili kubaini
wahusika.
Mwili wa Barlow ulifikishwa katika
Hospitali ya Rufaa ya Bugando kati ya saa 8.30 na tisa alfajiri na
kufanyiwa uchunguzi na madaktari na kisha kuhifadhiwa katika mochari ya
hospitali hiyo.
Mmoja wa madaktari ambao walimpokea
na kumfanyia uchunguzi wa awali walisema jeraha la risasi
lililosababisha kifo cha Kamanda huyo liliharibu mfumo wa mawasiliano
baada ya kumvunja shingo.
“Hakika ni moja ya vifo
vya kutisha ambavyo nimewahi kuvishuhudia tangu niwe daktari, hata
wenzangu tuliokuwa nao tulibaki tunashangaa kuona kiongozi mkubwa
anakatishwa maisha kwa risasi,” alisema mmoja wa madaktari ambaye
hakutaka jina lake liandikwe gazetini.
Baadhi ya wananchi waliozungumza kwa nyakati tofauti, walionesha masikitiko yao kutokana na kifo cha Kamanda Barlow.
Walisema
katika kipindi alichokaa hapa alifanikiwa kudhibiti ujambazi kutokana
na kusimamia doria za mara kwa mara jijini hapa na atakumbukwa kwa jinsi
alivyosimamia mauaji ya majambazi watano walivamia duka katikati ya
Jiji.
“Tumepoteza jembe halisi na mwana wa Tanzania,
Kamanda Barlow alifanikiwa kusimamia haki na kukomesha ujambazi,
tunaliomba Jeshi la Polisi mkoani hapa lihakikishe linawatia nguvuni
wahusika wote,” alisema Patricia Jumbe mkazi wa hapa.
Kaimu
Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Lily Matola alisema wanamshikilia mwanamke
aliyekuwa na Kamanda huyo kwa mahojiano ili kujua chanzo cha mauaji hao.
“Tunamhoji
mwanamke huyo na kufanya uchunguzi wa kina, tutatoa taarifa baada ya
kufanya uchunguzi wa awali na suala la mazishi tunasubiri maelekezo ya
kaka wa marehemu aliye Dar es Salaam,” alisema.
---
Sehemu hii ya taarifa imenukuliwa kutoka kwenye habari iliyoandikwa kwenye blogu ya Ziro & Tina