Thursday, September 20, 2012

WANAWAKE WA ARUMERU WAMUONYA MBUNGE NASSARI

Na Queen Lema, ARUSHA --  Wanawake wa eneo la Kisambare, Usariver, wilyani Meru mkoani Arusha wamesema kuwa kamwe hawatavumilia kauli za mbunge wa jimbo hilo, Joshua Nasari badala yake watalazimika kuingia barabarani kumpinga hadharani  Mbunge huyo  kwani kauli zake hazijengi hoja za kutetea shida za wananchi na badala yake zinachochea malumbano pamoja na migogoro huku wanawake wa Vijijini wakiwa wanakabiliwa na shida mbalimbali

Wanawake hao waliyasema hayo jana Wilyani humo wakati wakizungumza na Viongozi mbalimbali ambao waliwatembelea Kijijini humo sanjari na kuongea na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi.

Walisema kauli za Mbunge wao siyo za kujenga bali ni kubomoa na kuchochea malumbano makubwa ambapo kwa sasa alipaswa kuwa anaongelea jinsi ya kutatua changamoto mbalimbali zilizomo kwenye jamii.

Wakasema Mbunge huyo anapaswa kujua na kutambua kuwa alipewa jimbo hilo kwa hasira kutokana na kukithiri kwa changamoto lukuki ambazo zimo kwenye jamii hasa za Wameru na kwa hali hiyo huu ndio muda muafaka wa Mbunge huyo kuhakikisha kuwa anatatua kero na wala sio kutoa matammko ambayo hayana tija na jamii.

Waliongeza kuwa kauli hizo zimekuwa na madhara makubwa sana hasa kwa vijana kwa kuwa mpaka sasa wapo baadhi yao wanaofanya makosa na kuvuruga amani, kwa visingizo vya Mbunge huyo, “tunachotaka kujua ni kuwa tunatatuliwa kero zetu lakini badala mbunge afikirie suala zima la maendeleo yeye anafikiria kuzima mwenge wakati sisi hatuna shida na mwenge na mwenge unapita lakini shida zetu hasa sisi wakina mama wa Nkoakirika hatujui hata majira ya saa sasa tueleweje kwani tukimbia CCM kutokan a na changamoto lakini hii ya sasa ni kali na kama huyu mbunge ataendelea hivi basi ipo siku matatizo makubwa sana yatatokea” waliongea akina mama hao huku wakilia.

Mbali na hayo, waliongeza kuwa nao viongozi wa siasa watakiwa kukumbuka ahadi mbalimbali ambazo wamezitoa kwa jamii hasa nyakati za kampeni kwani baadhi ya viongozi, hasa wa Mkoa wa Arusha wakishapata nafasi ya kuongoza basi wanakuwa na matamko ambayo hayana tija na badala yake yanasabahbisha baadhi ya vijana kukamatwa ovyo na Polisi.

Awali Katibu wa CCM Wilaya ya Meru, Langaeli Akyoo alikiri kuwa CCM ilikuwa na kasoro hali ambayo iliwafanya wananchama wake kukopesha jimbo la Arumeru Mashariki lakini kwa sasa chama hicho kimejipanga hata kwa Watendaji wa huduma zote za kijamii kuhakikisha kuwa wanatekeleza sera za wananchi.

Bw. Akyoo alisema, hasira ambazo ndio chanzo  pekee cha wananchi kutoa kura kwa upinzani kwa sasa zitapunguzwa kwa kiwango cha juu  huku jamii hasa za vijijini zenye mahitaji maalumu nazo zikiweza kupatiwa ufumbuzi wa matatizo yao  kwani uwezekano wa kuwasaidia bado ni mkubwa sana.