Friday, September 28, 2012

AMWAGIWA MAFUTA YA MOTO KWA KULA KIPORO CHA WALI.

Ndugu na majirani wa Neema John wakijitahidi kumpepea Neema akiwa ndani ya gari kusubiri fomu ya Polisi  katika kituo cha polisi buguruni baada ya kumwagiwa mafuta ya moto mwilini na Dada yake Monica John katika ugomvi wa kugombania kiporo cha ubwabwa leo asubuhi.

Kwa mujibu wa mashuhuda tafrani hiyo ilitokea leo asubuhi katika eneo la Tabata kisiwani kwa kipingu baada ya Monica kudai kiporo cha wali kilichobaki jana ili aweze kukitumia kama kidfungua kinywa ambapo alielezwa na nduguye kuwa ameshakila ndipo ugomvi ukaanza na kufikia kumwagiana mafuta.

Kufuatia tukio hilo Monica alikamatwa na askari wa jeshi la Polisi wa kituo cha Polisi Tabata kisiwani na kufikishwa buguruni kwa hatua zaidi ambapo ndugu yake amelazwa katika hospitali ya Mwananyamala