Thursday, August 30, 2012

CWT WAITAKA SERIKALI KUTOPUUZA AMRI YA MAHAKAMA


Raisi wa Chama cha walimu CWT Gratian Mukoba (kushoto) wakijadiliana jambo na  Mkuu wa Idara ya Elimu na Mafunzo Bw, Anthony Mtavungu.
Chama cha walimu nchini Tanzania kimetoa wito kwa serikali kuacha kupuuza amri ya mahakama ikiwa ni pamoja na kuwahurumia walimu  kwani walimu wanamaisha magumu hivyo wanahitaji kusikilizwa na muajiri wao ili wapate mishahara inayokidhi mahitaji yao.

Akizungumza na waandishi wa habari leo katika makao makuu ya Chama hicho jijini Dar es Salaam Rais wa Chama hicho Bw, Gratian Mukoba  amesema kuwa Kitendo cha serikali kukaa kimya kwa muda wa siku 27 bila ya kuonyesha kujali kutekelezwa kwa amri ya mahakama iliyokuwa inaitaka serikali kufanya mazungumzo na walimu chini ya mshauri mtaalamu wa sheria za kazi ni dhahiri kwamba, serikali haoina nia njema  ya kusikiliza madai ya walimu.
Bw Mukoba amesema kuwa, tayari wameiandikia barua serikali lakini mpaka sasa hamna jibu lolote wala nia iliyoonyeshwa na serikali ya kutaka kukaa mezani kufanya majadiliano kama walivyoagizwa na mahakama.
Kufuatia malalamiko ya CWT chama hicho kimeitaka serikali  kuhakikisha kuwa mazungumzo kati yao na Serikali  kuwa  yanaanza kusikilizwa kabla ya shule kufunguliwa tarehe 10 september 2012 na pia Serikali ihakikishe kuwa walimu wote waliovuliwa madaraka kwa kisingizio kuwa wameshiriki mgomo wanarudishiwa vyeo  vyao vinginevyo chama kitaamini kuwa walimu wanapewa madaraka sio kwa uwezo wao bali kwa unyenyekevu uliovuka mipaka.
Baada ya mazungumzo na waandishi wa habari