Mama wa Msanii wa ngoma ya Number One, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura
Kasim ‘Sandra’ ameingilia kati penzi lililofufuka upya kati ya mwanaye
na staa wa filamu za Kibongo, Wema Sepetu.
Habari za chini ya kapeti zilitonya kuwa baada ya kuambiwa na kuoneshwa
picha za Diamond akiwa kimahaba na Wema alikuja juu akidai kuwa hamtaki
Wema kwa kuwa anamkubali zaidi Penniel Mungilwa ‘Penny’.
Akizungumza akiwa nyumbani kwake Sinza-Mori jijini Dar wikiendi
iliyopita, bi’mkubwa huyo alisema kuwa kwa sasa hafahamu chochote kuhusu
Diamond kurudiana na Wema zaidi ya kusikia kwa watu na kuona picha
katika mitandao ya kijamii.
“Kuhusu Nasibu (Diamond) kurudiana na Wema, nasikia tu na kuoneshwa
picha namsubiri Nasibu arudi kisha nikae naye ndipo nitatoa tamko,”
alisema mzazi huyo.
Mapaparazi wa Ijumaa Wikienda kadiri walivyozidi kumchimba mama mkwe
huyo wa Wema ni jinsi gani anavyojisikia kuhusu tabia ya kubadilisha
wanawake kama nguo, ikizingatiwa yeye ni mzazi haoni kama mwanaye
anamfedhehesha alisema kuwa hayo ni maisha yake.
“Hayo ni maisha yake na mwenyewe kwa kuwa ameshazoea kuonekana katika
magazeti kila wakati mi niongee nini wakati ndiyo maisha aliyojiwekea,”
alimalizia kusema.
No comments:
Post a Comment