Na Waitara Meng’anyi, Tarime
Ghati Chacha (21) mkazi wa kijiji cha Nyanitira kata ya Nyansincha Wilayani Tarime amesababishiwa kilema cha maisha kwa kukatwa mguu wake wa kulia na Mume wake baada ya kuchelewa kumfungua mlangao nyakati za usiku.
Akisimulua
mkasa huo hivi karibuni akiwa wodi namba sita alikolazwa akiuuguza
vidonda na majeraha,Ghati alisema, mume wake aliye mtaja kwa majina ya
Chacha Mwita(23) alifika nyumbani saa mbili usiku akiwa amelewa.....BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI»
“Aliniuliza
kwa nini nimechelewa kumfungulia mlango nikamjibu sikuwa nasikia,
baadaye akaniomba kurunzi na panga, nikamletea kurunzi na kumwonesha panga lilipo kwa kidole” alisema Ghati.
Wakati anamwonesa lilipo panga na kumpa kurunzi Ghati hakujuwa
kuwa nini kinafuata alifiki kuwa mambo ya wanaume pengine anataka
kwenda sehemu kwa kuwa ndizo tabia za wanaume wa maeneo haya kuondoka
usiku ama anataka kuangalia mji kama uko sawa alafu arudi kulala.
“ Alipoipata ile panga akaniambia leo atamitumbua utumbo, akaanza kunipiga kwa panga ile akanijeruhi sikio, mkono wa kushoto na mguu wa kushoto na kunikata mguu wa kulia ukakatika kama unavyoona” alieleza
kwa masikitiko akiifunua kanga iliyokuwa amejifunika akiwa amelala
kitandani hospitali ya Wilaya Tarime.
Wakati
anafanyiwa ukatili huo ali piga kelele lakini majirani hawakuwahi
kufika kumsaidia kwa kuwa ni kawaida ya mume na mke kugombana na vilio
kama hivyo kusikika katika maeneo hayo.
“Baadaye walikuja na aliposikia majirani wamefika alikimbia kwa kupitia mlango wa nyuma akitumia baisikeli yake, majirani walinifunga mguu
uliokuwa ukivuja damu na kunikimbiza katika kituo cha afya Muriba na baadaye kuletwa hapa” alieleza .
Hata hivyo mwanzoni Ghati alieleza kuwa chanzo cha matatizo hayo yote ni ndoa za mitala na unywaji wa pombe wa mume wake.
“
Nimeishi naye kwa miaka mine sasa na tuna watoto wawili na tulikuwa
tunaishi vizuri, tatizo akinywa pombe huonekana kama amewehuka linguine
ni baada ya kuoa mke wa pili ambapo alianza kunichukia , kuanza
kunipiga na sasa kunikata mguu” alisema Ghati.
Ghati hataweza kurudiana na mume wake huyo kwa kitendo
alichomfanyia kwa vile amesema hakioneshi utu na kuiomba mahakama imuhukumu
mumewe kifungo jera ili ajifunze
kutokana ukatili aliomfanyia.
”
Naomba serikali na watu binafsi wanisaidie magongo ya kutembelea kwa
kuwa sasa sina uwezo wa kuyanunua pia wanisaidie kusomesha watoto wangu
maana ni wadogo na mimi ndiye niliye kuwa nikitafuta tunakula”
alisema.
Wananchi
walioshuhudia kitendo hicho walionesha kusikitishwa na kukilaa kuwa
kinaendelea kuharibu jina la na sifa ya Wilaya ya Tarime .
“ Sikifurahii kitendo hiki kwani kinaonesha wazi ukatili wa hali ya juu kwa binadamu mwenzako na hii inasababisha hata watu ambao hawajawahi kufika huku kutuona sisi ni wanyama kumbe ni watu wachache wanaotuharibia sifa, mahakama imuhukumu huyu mtu adhabu kubwa inayomstahili ili liwe fundisho kwa wengine” alisema Mwita Machera aliyekuwa hostalini hapo.
Jeshi la polisi baada ya kupata taarifa lilifika lilifika eneo hilo la tukio na kushuhudia kipande cha mguu kama inavyoonekana kwenye picha hapa na kuamru kizikwe na juhudi za kumtia nguvuni kuanza.
Hata
hivyo siku mojs baadaye Chacha Mwita alikamatwa na jeshi la polisi kwa
kusaidiana na nguvu nza wananchi ambapo alifikishwa katika mahakama ya
Wilaya ya Tarime kujibu mashitaka hayo.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamishina masaidizi wa polisi kanda maalumu ya Tarime (ACP) Justus Kamugisha lisema kuwa baada ya
kuhojiwa Mwiata alikiri kumsababishia mke wake ukilema wa maisha.
“ Vitendo vya kikatili vilishapitwa na wakati, kumsababishia mtu ukilema wa maisha sii jambo lisilo la utu na linaonesha kuwa hakuna
ubinadamu kwa watu japo si wote” alisema Kamugisha kwa nija ya simu.
No comments:
Post a Comment