Tuesday, February 19, 2013

ZUZU YAAMUA KUING'OA SERIKALI YAO KWA KOSA LA KUUZA MLIMA VIDETE

WANANCHI wa Kijiji cha Zuzu Kata hiyo mkoani Dodoma, Wameiangusha Serikali ya Kijiji hicho iliyokuwa ikiongozwa na aliyekuwa Mwenyekiti Peter Mtawale (49) wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambaye ameamua kuiacha Ofisi yake kwa kosa la kuuza Mlima wa Widete.

Mtawale aliyezaliwa 1963 alikubali kujiuzulu kwa kuutangazia Mkutano wa Hadhara karibuni mwaka huu baada ya kubanwa na tuhuma nyingi ikiwemo ya kuuza Mlima huo kwa Mwekezaji ambaye alikiri Serikali yake ilimruhusu uchimbaji wa Rupia bila kuwaarifu wananchi.

Mbali ya Tuhuma za kuuza Mlima bila kuwataarifu wananchi na Uongozi wa Kata, nyingine ni pamoja na mauzo ya Changarawe (Kifusi), Maji, Mchanga,  Ufujaji  wa Fedha ya Malambo Mbgani, Ushuru wa Magari, kuingia kwa wageni bila taarifa, Kutoitishwa kwa Vikao na kusoma Mapato na Mtumizi, Milio ya Milipuko, na Viongozi kufunga Maji bila Mita.

“Kuna Uchochezi ninaofanyiwa na Diwani wa Kata Awadhi Abdalah (CCM), Mwenyekiti wa Changu (CCM) Omari Kagusi na Katibu Mwenezi Solo (CCM) ambapo 14.1.2012 walifanya kikao cha Siri kunijadili bila kunitaarifu,”alisema Mtawale alipohojiwa na kuonekana anafanya kazi zake kwa kuongozwa na Kigogo mmoja wa Kata anayempotosha.

Alipoulizwa kwa nini Serikali yake haikuwaarifu wananchi juu ya kuuzwa kwa Mlima huo hadi wakapatana Mwekezaji akipata anachochimba Mwekezaji atachukua asilimia 60% na Kijiji asilimia 40% alisema, kwa kuwa vikao vinakaa mara tatu kwa mwaka ilikuwa wawaarifu Machi, 2013.

Pamoja na kukiri kuingia mkataba huo mwezi Desemba 2012 alikubali walifanya makosa ya kutowaarifu wananchi na Uonozi wa Kata, lakini akasema Katibu Tarafa Joyce Malare ametumwa kutatua mgogoro huo lakini walishindwa kukaa hadi 21.1.2013 kutokana na koramu (akidi) kutokutimia.

Diwani Abdalah alipoulizwa alikiri kuwepo kwa Mgogoro huo na kusema yeye ametoa Taarifa kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ambaye amesema analifanyia Kazi, lakini alishangaa Katibu Tarafa kuanza kumuingilia akifanya Kazi za Kisiasa ili kumgonganisha na Wananchi Jambo alilosema hawezi kuvumilia na kukubali wananchi wadhulumiwe haki yao.

Aidha Katibu Tarafa Malare alipoulizwa na mwandishi amefikia wapi katika utatuzi wa mgogoro huo, hakuonesha ushirikiano na kuanza kumponda Mwandishi, “…nani kakwambia umbeya huo? ...Kwa utaratibu nikifanya kazi nampelekea mkubwa wagu siyo wewe!!”

Alimwagika maneno yasiyo na staha bila kujua Mwandishi alimhoji Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Lephy Benjamini juu ya mgogoro na kujibiwa anaushughulikia Malare.


No comments:

Post a Comment