Sunday, February 24, 2013

MNATANGAZIWA NAFASI ZA MAFUNZO YA UALIMU WA UJASIRIAMALI

NAFASI  ZA  MAFUNZO  YA  UALIMU  WA  UJASIRIAMALI.

NAFASI ZA MAFUNZO NA KAZI  (  MARCH  2013   INTAKE  )

(INTAKE  HII  NI  MAALUMU  KWA  WAOMBAJI  WANAOTAKA  KUWA  WAALIMU  WA  UJASIRIAMALI  KATIKA  MRADI  WA  ELIMU  YA  UJASIRIAMALI  MIJINI  &  VIJIJINI   KWENYE  WILAYA  WANAZO ISHI)

Taasisi  ya  RafikiElimu  Foundation   inapenda  kuwatangazia  vijana  wa  kitanzania  nafasi  za  mafunzo  na  kazi  kama  ifuatavyo :

KOZI  ITAKA YO  FUNDISHWA:   UALIMU  WA  UJASIRIAMALI.

SIFA   ZA  MWOMBAJI  NAFASI:

Awe   mtanzania    mwenye  umri  wa  kuanzia  miaka  18  hadi  45.
Awe   na  elimu  ya  kuanzia  kidato  cha   nne,  sita  na  kuendelea.
Aliye   na   utashi  na malengo  ya  kufanya kazi    kama  MWALIMU  WA  UJASIRIAMALI  kwenye  Mradi  Wa  Elimu  Ya  Ujasiriamali  Mijini  &  Vijijini.
Anayeweza  kusoma  na  kuelewa  kwa  njia  ya  masafa  marefu.
Awe  anaishi    katika  mojawapo  kati  ya  wilaya  zifuatazo ;  Arusha  Mjini,  Arumeru, Moshi  Mjini, Ilala,  Kinondoni, Temeke, Babati, Kigoma  Mjini, Bagamoyo, Kisarawe, Kibaha  Mjini, Nyamagana, Ilemela, Nansio-Ukerewe, Shinyanga  Mjini, Kahama,  Iringa Mjini , Njombe, Mafinga  Mjini,  Mtwara  Mjini, Morogoro   Mjini ,  Dodoma  Mjini,  Tanga  Mjini, Rungwe(  Tukuyu  ), Mbeya  Mjini, Tandahimba, Lindi  Mjini, na Mkuranga.

DHUMUNI   LA   KOZI HII:   Dhumuni  kuu  la  mafunzo  haya  ni  kuwaandaa  wahitimu  kufanya  kazi  kama  WAALIMU  WA  UJASIRIAMALI  katika  Mradi  Wa  Elimu  Ya  Ujasiriamali  Mijini  &  Vijijini  unaoratibiwa  na  Taasisi.

MUDA  WA  MAFUNZO: Mafunzo  haya  yatafanyika  kwa  muda  wa  miezi  mitatu.  Mwezi  mmoja  utakuwa  ni  mafunzo  kwa  njia  ya  nadharia  na  miezi  miwili  itakuwa  ni  mafunzo  kwa  njia  ya  vitendo  ambayo  yatafanyika  mashuleni na   kwenye  vituo  vya  mafunzo ya  ujasiriamali.

BAADA  YA  KUHITIMU: Wahitimu  wa  mafunzo  haya, watapata  nafasi  ya   kufundisha  somo  la  Ujasiriamali   mashuleni  na  katika  vituo   vya  ujasiriamali  vilivyopo  katika  wilaya  zao. .

ADA  YA  MAFUNZO: Ada  ya  mafunzo  haya  maalumu  ni  shilingi  elfu     35   tu  kwa  mwezi.

Tuma  maombi   ya  fomu  ya  kujiunga  na  mafunzo-kazi  haya   kupitia  barua  pepe yetu  ambayo  ni :  rafikielimutanzania@gmail.com

Maombi  yaelekezwe  kwenda  kwa  :

Mkurugenzi  Mtendaji,
RafikiElimu  Foundation,
Centre  For  Distance  Learning  Programme.
S.L.P  35967,
Dar  Es  salaam.

Mwisho  wa  kupokea  maombi  ni  tarehe  08 MACHI   2013.

Mafunzo  yataanza, tarehe 14    MACHI    2013.

N.B:  Tutachukua  wanafunzi  wachache  kutoka  katika  wilaya  tajwa  hapo  juu,  hivyo  idadi  ya  wanao  hitajika  ikikamilika  mapema, tutasitisha  kupokea  maombi  mapya.

Kwa  maelezo  zaidi, tembelea:  rafikielimu.blogspot.com

No comments:

Post a Comment