Tuesday, December 11, 2012

TASWIRA ZA MDAU MWANAKOMBO JUMAA KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 51 YA UHURU WA TANZANIA BARA

Kikosi cha Jeshi la Kutuliza ghasia FFU kikipita kwa ukakamavu wakati kikitoa heshima zake kwa Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Kikwete hayupo pichani katika  sherehe za maadhimisho ya miaka 51 ya Uhuru wa Tanzania Bara kwenye uwanja wa Uhuru  Oktoba 9 jumapili iliyopita  . Rais Kikwete  alikagua gwaride  la maadhimisho hayo lililoundwa na askari kutoka majeshi ya ulinzi na usalama lilionyesha umahiri mkubwa wa ukakamavu. (Picha na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO)
Kikundi cha halaiki chenye watoto 2,625 kutoka Tanzania Bara na Visiwani kikionesha sura mbalimbali ya  kitabu, ugonjwa wa mapambano dhidi ya malaria, nchi yangu Tanzania ,miaka 51 ya UHURU, Maliasili na Utalii.. (Picha na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO)
Kikundi cha ngoma cha Taifa kutoka Rwanda kikionyesha umahiri wake wakati wa maadimisho  ya miaka 51 ya Uhuru a Tanzania Bara jana katika Uwanja wa UHURU jijini Dar es Salaam, ambapo Rais Kikwete aliwashukuru wasanii  hao kwa kuja Tanzania  katika maadhimisho.(Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO).

No comments:

Post a Comment