MKUU
wa wilaya ya Muheza mkoani Tanga, Subira Mgalu, amemuweka rumande
Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ngomeni wilayani hapa Edmund Zongwe, kwa kosa
la kumsomea taarifa ya uongo kuhusu maendeleo ya kata hiyo.
Ofisa mtendaji
huyo alikamatwa juzi mchana na mkuu wa kituo cha polisi Mkanyageni na
kupelekwa katika kituo kikuu cha polisi Muheza mjini
Hatua ya kukamatwa Ofisa
mtendaji huyo wa kata imekuja baada ya mkuu huyo wa wilaya kutoridhika
na taarifa ya maendeleo ya kata kutoka kwa Afisa mtendaji huyo.
Alisema kuwa kutokana na hilo lazima Ofisa mtendaji huyo akawekwe rumande siku moja, akitoka bado atakuwa nakesi.
Hata hivyo, mkuu huyo wa wilaya
wakati akizungumza naye alimhisi mtendaji huyo kuwa amelewa baada ya
kusikia harufu ya pombe ambapo aliagiza akapimwe katika hospitali Teule
kama ili kubaini kama kweli amelewa.
Kutokana na agizo hilo Ofisa
mtendaji huyo alichukuliwa ndani ya gari la DC huku akiwa na mkuu wa
Kituo cha Polisi Mkanyageni na Daktari wa kituo cha Afya Mkanyageni hadi
hospitali Teule kwa ajili ya kupimwa.
Baada ya kufika huko alitolewa
damu, walirudi kutoa majibu ambapo ilielezwa kwamba hospitali ya Teule
haina kipimo kinachoweza hali hiyo ya ulevi au la hivyo damu hiyo
kuahidiwa kuwa itapelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ama KCMC
Moshi.
No comments:
Post a Comment