Wednesday, December 12, 2012

MAABARA YA KISASA ILIYOTAMBULIWA KIMATAIFA YATAMBULIWA RASMI NA WAZIRI WA AFYA TFDA


Mkurugenzi Mkuu wa  Mamlaka ya Chakula na Dawa Nchini  Bw, Hiiti Sillo akitoa maelezo ya Awali na kumjulisha Waziri wa Afya  juu ya Maabara ya TFDA kutambuliwaa kimataifa kwa  kupewa Cheti cha Ithibati kupitia Barua ya Tarehe 21 Septemba 2012.

Waziriwa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt,Hussein Mwinyi leo ameitambulisha Rasmi Maabara ya Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA  ya Chakula na Microbiolojia  baada ya kupata ITHIBATI kutoka  Southern African Development Community Accreditation Services  (SADCAS) iliyotolewa tarehe 19 September 2012.

Dk Mwinyi  ameipongeza TFDA kwa kuonyesha juhudi zilizopelekea upatikanaji wa ITHIBATI hiyo amapo amessema kuwa  anahukakika kuwa afya za Watanzania zitalindwa kupitia huduma za Maabara zenye uhakika.
Maabara hiyo ni Miongoni Mwa Maabara chache Barani Africa zilizopata ITHIBATI  kutoka  SADCAS katika uchunguzi wa Kimaabara lakini pia ni Maabara ya kwanza ya Chombo cha Udhibiti kupata ITHIBATI  kwenye nchi za Afrika Mashariki.


Mgeni Rasmi akifungua cheti cha kuashiria utambulisho wa Maabara hiyo.


Wakurugenzi wa TFDA wakiwa kwenye picha ya Pamoja na Mgeni Rasmi ambaye ni waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii.


Wafanyakazi wa TFDA nao walipata fursa ya kupiga picha na Mgeni Rasmi.



Baada ya Kumaliza kutoa Tamko Waziri wa Afa aliondoka hapo katika makao makuu ya TFDA na kuacha sherehe ikiendelea.  

No comments:

Post a Comment