Waombolezaji katika mazishi hayo hawakuruhusiwa kuuona mwili wa marehemu kwasababu ambazo hazikuweza kufahamika maramoja bali kilichoruhusiwa kuangaliwa
ni picha yake iliyokuwa juu ya Jeneza.
Marehemu Mwasokwa alikutwa na umauti baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana wakamkata na kitu kinachosadikiwa kuwa na ncha kali kisogoni
ambapo mwili wake ulikutwa umelazwa kifudifudi nje ya geti la nyumba yake eneo la Block T jijini Mbeya.
Taarifa za Jeshi la Polisi mkoani Mbeya, zimesema kuwa wauaji
wanaonekana kuwa walitumia panga, ambapo marehemu alikutwa na majereha makubwa
sehemu za shingoni, kichwani, mabegani na mkono wa kushoto.
Kwa hisani ya Kalulunga
No comments:
Post a Comment