TANZANIA IMESEMA IPO TAYARI KUPELEKA WANAJESHI 800 DRC
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa, Bernard Membe, amesema Tanzania iko tayari kupeleka kikosi
cha askari wake 800 kwenda kupambana na waasi wa Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Kongo (DRC), maarufu kama M23.
Ameyasema
hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa haari ambapo amesema kuwa
askari hao watajiunga na wengine kutoka nchi za SADC ili wafike 3200
kwa ajili ya jukumu hilo.
Amesema
kuwa Wanajeshi hao watasaidia kwenda kulinda mipaka ya DRC na kuzuia
baadhi ya miji inayotekwa na waasi wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
(M23) ambapo mpaka sasa tayari wameshauteka mji wa Goma.
No comments:
Post a Comment