Saturday, May 18, 2013

WAPENTECOSTE WAPINGANA NA IMANI ZA JUKWAA LA WAKRISTO TANZANIA


Mchungaji wa Kanisa Moja wapo la Kipentecoste akichangia Mada ambapo alisema kuwa ili swala la Migogoro ya Kidini iishe kinachotakiwa ni kuungama kwa niaba ya Tanzania Nzima.


Jumuiya ya  Makanisa ya Kipentecoste Tanzania,  wamejiondoa katika Jukwaa la wakristo Tanzania na kusema kuwa sababu za wao kujiondoa katika Jukwaa hilo ni kutokukubaliana Ki Imani.
Akizungumza katika Mkutano wao jana uliofanyika katika Hoteli ya Peacock jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti  wa Jumuiya hiyo, Askofu Pius Erasto Ikongo ambaye ni Askofu wa Makanisa ya Mirracle Church in Tanzania amesema kuwa sababu kubwa ya wao kutokukubaliana na  Jukwaa hilo TCF, ni kwamba  hawana Mitazamo sawa ya Kiimani.
Amesema kuwa, sio kweli kwamba, Wakristo wote wamekubaliana kwamba swala la Kugawana Mabucha likubaliwe kwa upande wao hawajashirikishwa na hivyo wamesema kuwa wao Wapentecoste wanapingana na jambo hilo la kugawana Mabucha.
Askofu Ikongo amesema kuwa, wanamuomba Rais Kikwete aingilie kati swala la kuchinja kwa kurejea kauli ya zamani ya Rais wa awamu ya Pili mzee Alli Hassan Mwinyi ya kuruhusu kila mtu achinje na ale kivyake.
Kwa upande wake, Makamu mwenyekiti katika kikao hicho, ambaye ni Askofu Mkuu wa Pentecoste Renewal Assembly Wilson Mwafululila, amesema kuwa, kitendo cha kukataza Mihadhara ya Kidini wao kama Wapentecoste hawaliungi mkono kwani Mihadhara ni sehemu ya Mahubiri kwao.

Mwenyekitiwa kikao kilichowakutanisha wajumbe wa Kipentecoste Tanzania AskofuPius Erasto Ikongo (kushoto) aliyavalia koti jeupe akisikiliza mada kwa makini kutoka kwa wajumbe waliohudhuria kwenye Mkutano huo jana jijini Dar es Salaam. kulia ni Mjumbe wa Umoja wa Wapentecoste.

Askofu Mkuu wa Pentecoste Renewal Assembly akizungumza na waandishi wa Habari juu ya wao kujitoa katika Jukwaa la Wakristo Tanzania.

No comments:

Post a Comment