Friday, May 10, 2013

WAMILIKI WA BAR NA MIGAHAWA WAPATIWA SOMO NA TRA

Mwelimishaji Mwandamizi Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA akijibu swali kutoka kwa mmoja wa wamiliki wa Mgahawa leo katika Seminar iliyofanyika katika Hoteli ya Bluer Pearl jijini Dar es Salaam.


Wafanya Bihashara wa Migahawa pamoja na Bar leo wamepatiwa Seminar juu ya umuhimu wa matumizi ya Kifaa cha kielectroniki cha kulipia Kodi.
Akiwaelimisha katika Seminar Hiyo iliyofanyika leo katika Hoteli ya Blue Pearl jijini Dar es Salaam, Mwelimishaji Mkuu Mwandamizi wa TRA Bw, Hamisi Lupenja amesema kuwa, lengo la kukutana na Wafanya bihashara ao ni Muendelezo wa wao kutoa Elimu kwa wafanya bihashara juu ya Umuhimu wa kulipa Kodi kidigitali.
Kwa upande wao wafanyabihashara na wamiliki wa Migahawa wameonekana kufurahia Kifaa hicho kwani wamesema kuwa kitawasaidi wao kujua kuwa Kodi zao zinafika mahali husika na hivyo kuwaondoa hofu, juu ya kuliwa kwa kodi zao.
Hamza Abdallah ni Mfanyabihashara anayemiliki Bar eneo la Tandika jijini Dar es Salaam, ambaye amesema kuwa, wafanyabihashara wengi wanakwepa kulipa Kodi  kwa kuhofia kuzidisha hela nyingi au kupunguziwa lakini baada ya kifaa hicho kuanza kutumika kitamsaidia mfanya bihashara kujua kabisa kuwa kodi yake inafika Mahali husika.


No comments:

Post a Comment