Monday, May 20, 2013

PICHA JINSI MBUNGE MSIGWA ALIVYOFIKISHWA MAHAKAMANI LEO NA BAADAYE KUACHIWA KWA DHAMANA


Mbunge Msigwa akishuka katika gari hilo la polisi tayari kwa kuelekea chumba cha mahakama
Mbunge Msigwa akiwa na gazeti mkononi baada ya kufikishwa mahakamani leo
Watuhumiwa wengine wa vurugu za machinga na polisi wakishuka katika karandinga la polisi


Wakili wa Msigwa kulia akiteta jambo nje ya mahakama 
WATUHUMIWA 60 wa vurugu kati ya machinga na polisi mjini Iringa akiwemo Mbunge  wa  Jimbo  hilo, Mchungaji Peter Msigwa, kwa sasa  wanafanyiwa  utaratibu  wa  dhamana  baada ya mahakama  kukubali  kupewa  dhamana. 
 Awali watuhumiwa  walisomewa mashitaka matatu  huku mbunge  akisomewa shitaka la  kushawishi  watuhumiwa hao kufanya  vurugu.
  
Watuhumiwa  wote  wamekana mashitaka  dhidi yao na kwa  sasa utaratibu  wa dhamana  unafanyika mbele  ya mahakama ya  hakimu mkazi  wa wilaya ya  Iringa, Mheshimiwa  Godfrey Isaya.



Mashitaka waliyosomewa watuhumiwa ni pamoja na shitaka la kwanza la mbunge ambalo ni kushawishi kufanya vurugu, huku  wengine  wote  makosa yao yakiwa ni kufanya mkutano bila kibali, kuharibu mali kinyume na sheria ni  kufanya  vurugu.
 
Kada wa Chadema Frank Mwaisumbe akiingia na viongozi wengine wa chadema mahakamani hapo huku wafuasi wao wakizuiwa nje ya mahakama
Wafuasi wa Chadema wakiwa wamezuiliwa nje ya viwanja vya mahakama kuu kanda ya Iringa wakati mbunge alipofikishwa katika mahakamani mchana huu
Ulinzi mkali kweli kweli

No comments:

Post a Comment